Je, ni Ba? Mane? Cisse? Kuna wachezaji wazuri sana kutokea Afrika Magharibi ambao wamepamba sana michuano ya Ligi Kuu ya Uingereza.
Hakika wana vipaji vikubwa sana na wameweza kufanya vyema wakiwa ndani ya Premier League.
Kwa leo tutaangazia wale waliotokea kwenye taifa la Senegal. Jumla ya wachezaji 37 wameshiriki mashindano hayo wakitokea Senegal. Mtu mmoja maarufu zaidi ni Aly Dia ambaye alikuwa wa kwanza kuiwakilisha nchi yake kupitia klabu ya soka ya Southampton mwezi Novemba mwaka 1996.
Cheikhou Kouyate, Sadio Mane, Ismaila Sarr na Oumar Niasse nao wamefanya hivyo hivyo msimu huu.
Mfungaji wa hatitriki ya mapema zaidi ndani ya Premier League, Mane alijitengenezea jina lake akiwa na Saints kabla hajahamia kwa Liverpool.
Yeye alikuwa ndiye mchezaji mmojawapo kati ya wachezaji watatu walionyakua tuzo ya Golden Boot katika msimu wa 2018/19 mara baada ya kupachika jumla ya magoli 22 na akasaidia upatikanaji wa mabao 29 huku akifunga mabao 80 kwa ujumla, hii ni zaidii ya mchezaji yeyote kutoka nchini kwao.
Kuna mabao bora sana yaliyofungwa ndani ya PL kwa kupitia mastaa kadhaa wa kutokea Afrika Magharibi akiwemo Sadio Mane, Papiss Cisse na Demba Ba
Demba Ba amefunga magoli 43 kwenye michuano hiyo na kushinda tuzo ya Premier League Player of the Month mwezi wa kumi na mbili mwaka 2011 akiwa na klabu ya soka ya Newcastle United, kabla hajahamia kwa Chelsea.
Papiss Demba Cisse aliwika sana akiwa pale St James’ Park, akapachika jumla ya mabao 13 katika mechi 14 alizocheza tangu ajiunge na klabu hiyo mwezi Januari mwaka 2012 na akawasaidia The Magpies kumaliza msimu wakiwa nafasi ya tano.
Angalia takwimu za wachezaji wa Senegal
| Mechi | Magoli | Assists | |||
|---|---|---|---|---|---|
| El Hadji Diouf | 243 | Sadio Mane | 80 | Sadio Mane | 29 |
| Mohamed Diame | 239 | Demba Ba | 43 | El Hadji Diouf | 25 |
| Cheikhou Kouyate | 187 | Papiss Demba Cisse | 37 | Cheikhou Kouyate | 10 |
| Sadio Mane | 185 | Henri Camara | 31 | Mame Biram Diouf | 9 |
| Abdoulaye Diagne-Faye | 166 | El Hadji Diouf | 28 | Henri Camara | 8 |
Idrissa Gueye alikuwa ni mchezaji muhimu sana kwa Aston Villa pamoja na Everton, akiwa na umaridadi sana awapo uwanjani kwenye gemu zake alizocheza.
Mido mwenzake, Mohamed Diame alicheza mara 239 kwenye Premier League kwa klabu za soka za Wigan Athletic, West Ham United, Hull City na Newcastle, akiwa wa pili kutokea kwa El Hadji Diouf miongoni mwa wenzake wanaotoka taifa moja.
Ni nani aliwika sana ama anawika sana kwenye ligi akitokea huko Senegal?
- Demba Ba
- Papiss Demba Cisse
- Mohamed Diame
- Idrissa Gueye
- Sadio Mane


Gabriel
Good news 👍
Neema juma
Waoooo safi sanaa
Elika
Safiiiii
aisha
mane ni jembe la kila mtu
povel
mane is best soon atachukuwah mchezaj bora wa dunia
Kenani
Yuko pamoja
Mwajuma
Mane jembe namkubali sana
mwakalosi
Kwangu El hadji diof ndio mchezaj bora mpaka sasa
Tatu
Namkubali money
samiah
👍👍
Ernest Kimeru
Demba cisse is a phenomenal!!!
Hopemwaikux
🙌
Frank patrick
Sadio Mane
Winfrida
Mane ni kiboka
Aziza mushi
Vizuri 🤙
Mwanahamisi
Mane anatisha sana
Agness
Mane ni jembe kali
Warda
Sadio mane ndo namkubali
Njiku
Sadio mane the best player in senegal
Furahav
Mane noma.
Lydia Emmanuel Magoti
Safiii sana
Adelta
👍👍
Genia Sikaluzwe
Habari njama hiii