Baada ya ulimwengu kufikwa na janga hili la virusi vya Corona, kumekuwa na changamoto nyingi na kukwama kwa shughuli nyingi duniani. Shughuli za utamaduni, uchumi, utalii, kazi za kijamii na hata michezo vile vile. Ni lazima Kuchangia?
Pigo hili kwa ulimwengu, ambalo limesababisha vifo vya watu wengi na kuzidiwa kwa mifumo ya Afya ya Umma, limefanya wadau wengi kuungana na kufikiria namna ambavyo wanaweza kutoa mchango wao kuinusuru mifumo ya Afya na kuokoa maisha ya watu wengi.
Wito umetolewa kwa mastaa wa soka kuchangia, kama ambayo baadhi ya wafanya biashara mashuhuri kama Jack Ma, walivyotoa michango yao. Sawali linakuja ni namna au mfumo upi bora wa uchangiaji unahitajika ili kumgusa kila mchezaji wa soka la kulipwa.
Wadau wengi wanatofautiana mawazo hapa. Mfano, Ligi Kuu ya England ilishauri kupunguzwa kwa mishahara kwa asilimia 30 kwa wachezaji ili kushiriki kupunguza athari za virusi vya Corona kiuchumi katika klabu. Baadhi ya Ligi pia kama Hispania na Italia nao wameona kama ni vyema wakifanya hivyo, kupunguza athari.
Lakini changamoto ni kuwa sio wachezaji wote wanalipwa sawa. Pia kila mtu ana majukumu yake kiasi kwamba licha ya kuwa na wito wa kutaka kuchanguia kwa namna yeyote, punguzo la mshahara kwake ni pigo kubwa. Baadhi yao wanahudumia familia kubwa na wategemezi wengi, hivyo kuamua kuwakata wote paomja kunaweza kuwasababishia shida wengine.
Mtazamo Wanasoka Kuchangia
Bila shaka kila mwanasoka ana wiwa kutoa mchango wake kulingana na hali yake na namna anavyohisi itampendeza na kumuacha katika uafadhali pia wakati dunia nzima ikipambana.
Sio wachezaji wote ni mabilionea au mamilionea kwa kulingana vipato, maana wapo wachezaji wengi maarufu wakiwa na vyanzo vingine vya pesa zaidi ya wengine.
Hivyo ni heri kila mwanasoka akapewa nafasi binafsi ya kuchangia kwa kusaidia mashirika au taasisi za Afya zinazopambana kutatua hili. Kutoa mchango kwa waathirika au wagonjwa kwa namna yeyote inayompendeza na rahisi.
Ester jackson
Sio lazima baadhi yao wanahudumia familia kubwa na wategemezi wengi, hivyo kuamua kuwakata wote paomja kunaweza kuwasababishia shida wengine.