Beki wa Wolfsburg, Maxence Lacroix akizungumzia kuhusu tetesi zinazomtaja kutakiwa na Chelsea.

Maxence amesema: “Hizo tetesi nimeziona lakini nimeziacha zishughulikiwe na mtu anayenisimamia kwasababu nataka nielekeze akili yangu kwenye kazi yangu hapa Wolfsburg na nataka nifanye kazi nzuri nikiwa hapa.”
“Bado nipo na Wolfsburg na tumeshafuzu kucheza Ligi ya Bingwa Ulaya. Nina furaha sana kuwa hapa. Bado nina mkataba wa miaka mitatu na nimeridhishwa kuwa hapa.”

“Ni kweli kwamba mambo yanaweza kutokea kwa muda mfupi kwenye soka lakini bado najiona nina nafasi na nipo sawa kuendelea kubaki Wolfsburg na sijaona kama kuna sababu ya kuwaza mahali pengine.”|
Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.



Sarah
Asante kwa taarifa