Nina Mabeki Wawili wa Kuziba Pengo la Lamine Moro -Luc Eymael

Kocha Mkuu wa Yanga Luc Eymael raia wa Ubelgiji amefunguka kuwa hakutakuwa na pengo lolote la kumkosa beki wake wa kati Lamine Moro kwenye mechi atakazokuwa nje kwa sababu ana zaidi ya wachezaji wawili wa kuziba nafasi hiyo.

Kocha huyo ameongeza kwamba tayari ameshawaandaa Kelvin Yondani, Andrew Vincent,’Dante’ na Ally Mtoni, ‘Sonso’ kwa ajili ya kuziba nafasi ya beki huyo Mghana.
Lamine amefungiwa kucheza mechi tatu za Ligi Kuu Bara na kamati ya utendaji kutokana na kosa la kumrukia kwa makusudi na kumpiga teke kiungo wa JKT Tanzania, Mwinyi Kazimoto ambaye naye amefungiwa mechi tatu.
Eymael amesema kuwa hakutakuwa na pengo la Lamine hata kidogo kwa sababu wachezaji hao wawili ambao ni pamoja na Ally Mtoni ‘Sonso’  na Kelvini Yondani wanaweza kutumika katika nafasi hiyo na kucheza vizuri.
“Kwanza kuhusu Lamine ni mchezaji mzuri na ambaye nimemtumia sana kwenye mechi zetu lakini naona kukosekana kwake wala haitakuwa tatizo kubwa.
“Nasema hivyo kwa sababu Yondani amekuwa kwenye fomu ya hali ya juu, kwa hiyo anaweza kucheza na Makapu (Said) na wakawa na muunganiko mzuri tu kwenye mechi zote ambazo tutamkosa.
“Lakini pia namrudisha Sonso (Ally Mtoni) katika kundi na ana uwezo wa kucheza hapo, pia usisahau kuhusiana na Dante ambaye naweza kumtumia pia. Kwa hiyo utaona kwa kiwango gani hakutakuwa na madhara ya kumkosa,” alisema Eymael.

43 Komentara

    Sikuzote kocha mzuri hua na mbadala wa mchezaji tokea mazoezini tunasubili matokeo mazuri tu kwa wanayanga

    Jibu

    Mabeki anoa wengi Ndio maana anatamba sawa tutaona Kama kweli wataziba pengo lake

    Jibu

    Wapo wengi mabeki ndio maana wanatamba

    Jibu

    Tutaona kama wataziba pengo lake

    Jibu

    Sijui itakuwaje gonja tuone Kama wataziba Hilo pengo

    Jibu

    kocha wa utopolo bhn kijimwambafai

    Jibu

    Yanga washafulia hawana jipya sasa

    Jibu

    Yanga hakuna timu.! #meridianbettz

    Jibu

    Atua nzuri kwa kocha huyu subiri tuone endapo kama watazaa matunda

    Jibu

    Hiyo ndio kazi yake kocha lazima hamtengeneze mchezaji mbadala..!mashabiki tunategemea matoke mazuri yanga afrika

    Jibu

    Asante meridianbet #kwa taarifa

    Jibu

    Ata kama anao wa kuziba pengo lakini hawawezi kumfikia kiwango chake kimpira

    Jibu

    Imekaa powa sana katika vita lazima upambane na pia kama silaha zimeisha kuna njia mmbadala za vita pambana kocha tunataka kuona matokeo tofauti sio kufugwa ukocha unaujua panga majeshi

    Jibu

    Yanga wamefuli sana sasahivi

    Jibu

    Yanga mbele zaidi…

    Jibu

    Yanga hamuna mambo tena mshafuria#meridianbettz

    Jibu

    mmmh hatar

    Jibu

    Ni kocha mzuri anajiandaa vizuri kwa kila tukio la upungufu wa wachezaji

    Jibu

    yanga mbele daima

    Jibu

    Yanga hamna kitu humo wajipange upya

    Jibu

    Dante anaweza kuziba gap vizuri. Yondani hawezi kuwa mbadala#meridianbettz

    Jibu

    Tunasubiri matokeo yako kocha naamini mambo yatakua mazurii

    Jibu

    Ngoja tuone pengo lale litaonekana au laah!!!!

    Jibu

    Tunasubili matokeo maneno mengi ya nini

    Jibu

    Goja tuone itakuwaje

    Jibu

    Upande wng Sina shaka na huyu kocha luc Eymael

    Jibu

    Ndio maana anatamba sawa tutaona Kama kweli wataziba pengo lake

    Jibu

    Yetu macho

    Jibu

    Yanga hamna jipya

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Yaani Hii Timu bwana huwa hata siielewi#Meridianbettz

    Jibu

    Daima mbele Nyuma mwiko…

    Jibu

    Ngoja tutaona maneno yake yanaukwelia au anazingua tu

    Jibu

    Wachezaji wa Yanga hawajitambui.

    Jibu

    Wanao mabeki wengne lkn pengo la lamine alinambadala makosa mengi

    Jibu

    Imekaa powa sana katika vita lazima upambane na pia kama silaha zimeisha kuna njia mmbadala za vita pambana kocha tunataka kuona matokeo tofauti sio kufugwa ukocha unaujua panga majeshi

    Jibu

    Kocha siku zote pengo alizibiki labda mbadala ndio unafanyika

    Jibu

    Sawa baba acha tuone itakuwaje maana sisi mashabiki ndio tutaona kama pendo litazibiki au laa?

    Jibu

    Upo vizuri kocha kwa kujiamin

    Jibu

    Maoni:Asante kwa taaria #meridianbettz

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.