Mshambuliaji nyota wa Tottenham Hotspurs, Harry Kane amesema kuwa kwa sasa anajisikia kuwa yuko vizuri kuliko kipindi chochote kile!
Kane jana amecheza mchezo wake wa 200 katika ligi kuu ya Uingereza huku akiisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya West Ham kwa goli lake la dakika ya 82 ya mchezo huo.
Mchezaji huyo ambaye ametoka kwenye majeraha ya muda mrefu, alionesha kiwango cha kuridhisha sana katika mechi hiyo kiasi cha kumvutia kila aliyepata nafasi ya kutazama mtanange huo.
“Nafikiri hiki ndicho mshambualiaji anapaswa kufanya, kufunga magoli na kuisaidia timu kuchukua alama tatu kwenye kila mchezo. Nafurahi kurudi katika orodha ya wafungaji leo”, alisema Kane katika mahojiano yake na kituo cha televisheni cha Sky Sports muda mchache baada ya mchezo huo kumalizika.
Kane ambaye alikua nje ya uwanja kwa zaidi ya kipindi cha nusu mwaka kwa sababu ya majeraha, alionesha kiwango kikubwa mno katik mechi hiyo tofauti na wengi walivyotarajia kwamba ingemchukua muda kiasi kuyazoea mazingira ya uwanjani tena.
“Niko poa zaidi sasa kuliko kipindi chochote kile, nilipata nafasi ya kupona na kupumzika kutoka kwenye majeraha”, akaongezea “Kufunga ni jambo linaloleta furaha sana duniani, imekua muda mrefu tangu nifanye hivyo kwa mara ya mwisho.”
Goli hilo la Kane katika dakika ya 82 ya mchezo, ni goli la 137 kwa Kane katika ligi kuu katika miaka 6 aliyocheza kama mchezaji wa kikosi cha kwanza.
Nyota huyo wa Tottenham ana malengo ya kufikisha jumla ya magoli 200 katika ligi ya EPL na hilo linaonekana li mbioni kuwezekana kama asipobughuziwa na majeraha ya mara kwa mara kwani mpaka sasa ana miaka 26 tu!


Evaluziga
Namkubali Sana uyu jamaa
David Pere
Jamaa anajiamini Sana Ndio maana Jana kawanyoosha vizuri kabisa
Dorophina
Kane yupo vizuri naamini atafanya vzr zaid
Mariam mtandama
Yupo vizur
Samiah
Mungu azindi kumpa nguvu
Elika
Safi sana Kane tunakupenda pia mashabiki
felister
vizuri Kane endelea kuwanyoosha
Isaya massawe
Ni mojawapo ya wachezaji muhimu na tegemezi pale Tottenham
Caroline
Kane chapa kazi
Antony Luseno
Huyu ndo mr spurs ataipa matokeo kuanzia sasa akirejea
Sadick
Ni mshambuliaji mzuri lakini kwa mfumo wa Mourinho kushambulia kwa kushitukiza anaweza asifikishe idadi hiyo ya magoli#meridianbettz
fatumakasom
Safi kune endelea kuwanyoosha
Ester jackson
Safii sana Kane mana nafikiri hiki ndicho mshambualiaji anapaswa kufanya, kufunga magoli na kuisaidia timu kuchukua alama tatu kwenye kila mchezo
Devotha
Hongera sana kane Mungu azidi kukupa nguvu
Gabriel
Kwa mujibu wa sky news wametudhibitishia kuwa Harry kane yuko poa kabisa n habar nyema sana kwetu pia tunashukuru meridianbet Tanzania kwa taarifa ambaye njema sana kwan kutokana na hal yake tulijua hatoweza kucheza mechi ya dhid ya Tottenham na west ham siku ya Jana hivyo kama mashabiki wa Hotspur tunafurahia kumuona jembe letu raia wa England kurud akiwa na afya njema tena kutudhibitishia hali yake yuko fiti tena sana n habar njema kwenu
maana tokea apatwe na majeraha takriban miez sita tuliamin atoweza kurud akiwa fiti kabisa ila no furaha kuona amerud akiwa yuko vzur zaid
Have a great news 👍
# meridianbet Tanzania
Zeiyana
Habari njema maana tokea apatwe na majeraha takribani miezi sita turijua kama hatoweza kurudi akiwa fiti kabisa
tumaini
Maoni:kane yuko vizuri na azidi kufanya vizuri
Amani
mfumo wa Mourinho kushambulia kwa kushitukiza anaweza asifikishe idadi hiyo ya magoli#meridianbettz
Tahiya
Harry Kane ni mchezaji mzur na jana amedhihirisha
Genia Sikaluzwe
Ni habari njema kwa mashabiki Tottenham
Hamidu
Talent player.meridianbettz
Magdalena
Kane ni mahili Sana katika mpira lakini anabidi atulie kwanza ajisikilizie afya yake zaidi ndo arudi katika soka
isha
Kane safi sana nakukubali makali wangu
Povel
Kane yupo POA sababu wanamatumain na profile ya Jose Mourinho ya kubeba mataji kila timu aliyopitah hivyo kane amamatumain kiu yake ya kubeba taj next season unawez ikatimiah kutokana na record ya Jose Mourinho ndo maana anajisikiah mtu mwenye fulan natumain lake kiu yake itakatwa msimu ujao kwa kubeba taji lolote baran ulaya thnks meridian bet kwa update za michezo
Issa
Ni mchezaji mzuri na anapokuwa langoni wma timu pinzani ni hatari mno
Mwanahamisi
Yupo vizuri
Mwajuma
Kwa mpira wajana kweli yupo vizuri
farida ahmadi
Hajaongopa kweli kabisah kane ni mchezaji mzuri Sana pia mchezaji bora na mwenye nidhamu Asante kwa habar nzuri meridianbettz
Angelina
Safiii
Shafii
Ni Jambo zuri ni kheri urudi dimbani maana tulimic vitu vyako Kane
Sabrina
Maoni:Harry Kane yuko vizuri jamaa anajua
Ester mmakasa
Mungu amjalie kane aendelee vizuri na azidi kufanya vizuri wakati wote.
Hope mwaikuka
Good to hear this
Njiku
Hakuna mwanasoka asiyejua kazi ya mshambuliaji huyo wa uingereza ambaye anaekipiga tottenham habari zuri kwa wapenzi wa soka na kwa mashabiki wa tottenham
Neema hassan
Kane fundii
Aziza mushi
Kene mshambuliaji mzuri Sana.💪
Omary lukumbi
Harry kane n mchezaj mzr wa kiingereza na timu ya taifa na club yake ya spurs
Ernest
Watu wengi wanatamani sana kumuona Kane akiwa fiti ndani ya dimba ili tuweze kupata burudani kamili
Amiri Kayera
Majeraha yalimzingua ila analijua Sana gori
Johnmary joel
Kujiamini ndo mpango mzima#meridianbett
Latifa juma mohamed
Kane natumania ni kiungo Bora Sana, natumai na zaidi km anenavyo atafanya vzr Sana.
Latifa juma mohamed
Natumania Kane ni kiungo Bora Sana km anenavyo nafsin amerjea vema kwa sasa naamin ataendeleza ubora wake Zaid.
mwakalosi
huu msimu apumzike tu
Samira
Ni mchezaji mzuri sana
Rehema
Yuko vizuri
Agness
Mchezaji anae jitambua
christopher
Naona Kane ameanza kufanya balaa
warda
Namkubali sana Kane#Meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Naona kane ameanza kufanya baraha
Khadija
Kane yupo vzr#meridianbettz
Emmy cleopa
Kane fundiii
Adelta
Kane uko vizuri
Mashabiki tunamkubali sana
Furahav
Kane namkubali sana.
Theonestina
Namkubali sana uyu jamaa
nasra
Kane anajua
Salma
Kane namkubal sana
Asia Abdy
Jambo jema kane yuko vzur