Mustakabali wa Victor Osimhen ulikuwa gumzo kuu katika kipindi chote cha uhamisho wa majira ya kiangazi huku kocha mkuu wa Chelsea Pochettino akimhitaji pia.
Mshambuliaji huyo wa Nigeria alifurahia msimu mzuri wa 2022-23 huko Napoli, kwa mabao yake 26 na mchezo mzuri wa pande zote ulioisaidia Partenopei kutwaa taji lao la kwanza la Serie A tangu 1990.
Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.
Nia ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 bado iko juu huku vilabu vingi vya Premier League na Saudi Pro League vikipanga kujaribu kupata saini yake anayoitamani siku zijazo.
Kocha wa Chelsea, Mauricio Pochettino amemuongeza nyota wa Napoli na Nigeria, Victor Osimhen kwenye orodha ya wachezaji wanaoweza kusajiliwa mwezi Januari.
The Blues hawana moto wa kuotea mbali katika safu ya ushambuliaji na wamefunga mabao 11 ya Premier League katika mechi nane hadi sasa msimu huu.
Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara.
Kulingana na ESPN, Pochettino ni shabiki wa Osimhen mwenye umri wa miaka 24, ambaye tayari amefunga mabao sita ya Serie A mnamo 2023-24.