Pitso Mosimane Aongeza Mkataba Mpya Al Ahly.

Kocha wa Al Ahly, Pitso Mosimane (57) ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia klabu hiyo ya Misri mpaka msimu wa 2023/24.

 

Pitso M. alitangazwa rasmi kuwa kocha mkuu wa klabu ya Al Ahly mnamo Oktoba mwaka 2020 akitokea ya kalbu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini.

Taarifa hii imethibitishwa na Al Ahly wenyewe ambao kupitia kurasa zao za kijamii na tovuti wametangaza juu ya mkataba huo mpya ambapo pia wasaidizi wa kocha huyo nao wameongeza mkataba wa miaka miwili.

Al Ahly inatangaza kumuongeza mkataba wa miaka miwili Pitso Mosimane kutokana na mafanikio aliyoyapata klabuni, ” ilisomeka taarifa hiyo.

“Mosimane na wasaidizi wake wamesaini mkataba mpya na klabu kuondoa tetesi mbalimbali zilizojitokeza kipindi kilichopita. “ Al Ahly waliongeza katika taarifa hiyo.

Pitso amekuwa na mafanikio na Al Ahly wakifanikiwa kutwaa Ligi kuu ya Misri, Kombe la Ligi na Ligi ya Mabingwa Barani Afrika mara mbili mfululizo katika kipindi cha misimu miwili alichokuwepo hapo.



VUNA MKWANJA NA SHINDANO LA EVOPLAY SPRING AWEKING

Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000  katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe