Polisi Tanzania Yapata Ajali Moshi

Klabu ya Polisi Tanzania imepata ajali leo asubuhi wakati ikitoka mazoezini kurejea kambini huko Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kwa mujibu wa shuhuda [hakutaka jina lake litajwe] ameeleza kuwa, gari liliacha barabara na kugonga mti maeneo ya jirani na Kiwanda cha Sukari TTC ambako ndio Polisi Tanzania FC hufanyia mazoezi yao na walikuwa warudi mjini [Moshi] ambako ndio kwenye makazi yao.

“Basi la Wachezaji wa Polisi Tanzania limepata ajali baada kuacha barabara na kugonga mti wakati likirudi kambini baada ya mazoezi. Kuna baadhi ya wachezaji wameumia vibaya lakini tayari wameshakimbizwa hospitali.”

Klabu hii yenye maskani yake pale Moshi imethibitisha kuwa mmoja ya wachezaji Gerald Mathias Mdamu aliyevunjika miguu. Tuwaombee wachezaji hawa wapone haraka na kurejea katika shughuli zao.


KUSANYA PESA HAPA!

IcyGems kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet. Ndio, ukiwa kwenye nyumba ya mabingwa, ndipo utakapoufurahia ubora wa Kasino ya Mtandaoni sambamba na kushinda kwa ushindi mkubwa! Ishi na hii, IcyGems!Meridianbet

INGIA MCHEZONI

Acha ujumbe