Rafael Varane Awakubali Man United

Beki wa Real Madrid, Rafael Varane ameripotiwa kuikubali Manchester United kuelekea msimu ujao 2021/22.

Kumekuwa na ripoti mbalimbali kuhusu uwezekano wa Varane kusajiliwa na United kwenye dirisha hili la usajili. Hii sio mara ya kwanza kwa United kuhusishwa na Varane, 2011 ilibaki sehemu ndogo kumuona Varane Old Trafford ila mambo yalibadilika baada ya kupokea simu ya Zinedine Zidane, wakati ule alikuwa mshauri wa Florentino Perez.

Miaka takribani 10, Rafael Varane amekuwa Madrid na sasa ameweka wazi kwa uongozi wa klabu hiyo kuwa anatakakupata changamoto mpya na EPL ndio sehemu anayotaka kwenda, Man United kwa msisitizo.

Varane ameshatwaa mataji 4 ya Uefa akiwa na Madrid

Japokuwa kulikuwa na ripoti kuwa United walipeleka dau la pauni milioni 50 ambalo lilikataliwa na Madrid, raisi – Florentino Perez amekanusha uhalisia wa kitendo hicho akisisitiza kuwa hawajapokea ofa yeyote inayomuhusu Varane. Japokuwa, lengo kubwa la Madrid ni kumbakiza beki huyo kwa kumpatia mkataba mpya ila kama anaweza wazi adhma ya kuondoka, huu ndio muda pekee ambao Madrid wanaweza kupata faida ya kumuuza Varane kabla hajaondoka kama mchezaji huru msimu ujao.

Changamoto kubwa inayoweza kutokea kwenye mchakato huu ni mshahara wa Varane. Inasemekana licha ya kuichagua United, Varane anataka mshahara wa pauni laki 4 kwa wiki. Huu utakuwa ni mshahara mkubwa kuliko mchezaji yeyote wa United na ni kitu ambacho Man United hawataki kurudi makosa waliyoyafanya kwa Alexis Sanchez miaka ya nyuma.


USHINDI BILA MIPAKA!

Hakuna mipaka ya ushindi kwenye Keno Instant ya meridianbet Kasino, hii wewe ndiyo una uamuzi zaidi juu ya mchezo na nafasi ya machaguo kibao.
Arsenal, Arsenal Wawasilisha Ofa ya Pili Joaquin Correa., Meridianbet

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.