Hatimaye, Manchester United wanakwenda kumpata kocha wa muda. Ni Ralf Rangnick, muasisi wa mfumo wa kijerumani.
Kama ulikua haumfaham, za chini chini zinasema, Ralf Rangnick ndio mwalimu wa Jurgen Klopp, Thomas Tuchel na Julian Niglesmann. Hawa ni miongoni mwa makocha wa Kijerumani wanaofanya vizuri sana kwenye ulimwengu wa soka.
Kama alivyo Marcelo Bielsa kwa Pep Guardiola, Rangnick anaheshimiwa sana na wanafunzi wake. Akiwa na umri wa miaka 69 kwa sasa. Rangnick anaitumikia Lokomotiv Moscow kama mkurugenzi wa michezo na maendeleo.

Wasifu wake kama kocha unaturudisha mwaka 2010/11 alipoifikisha Schalke 04 hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa (walifungwa na Manchester United) na pia, walibeba kombe la German Cup msimu huo huo.
Ralf Rangnick huyu huyu, aliiongoza RB Leipzig kwenye fainali ya mashindano ya German Cup mwaka 2019. Kuelekea mchezo wa Super Sunday dhidi ya Chelsea, United itaongozwa na Carrick wakati huu ambao taratibu za kumkabidhi kazi Rangnick zikiendelea.
Wiki nyingine ya kushinda mamilioni ukiwa na kasino maridhawa za meridianbettz. Mchezo pendwa wa Fai Cai Shen unakupa thamani ya dau lako, kwa kiasi kidogo cha dau unaweza kushinda mkwanja mrefu.


