mshambuliaji wa klabu ya Manchester United Marcus Rashford ameripotiwa kuanza mazoezi katika kiwanja cha mazoezi cha klabu hiyo cha Carrington baad ya kupata majeraha madogo.
Marcus Rashford aliibua mjadala mzito juu ya majeraha yake baada ya kujitoa kwenye timu ya taifa ya Uingereza, Huku taarifa ikitoka ndani ya klabu hiyo kua mchezaji huyo alipata majeraha madogo lakini jana ameonekana akifanya mazoezi Carrington.
Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza ilielezwa kutokufurahishwa na mchezaji kujitoa kwenye timu hiyo baada ya kuitwa kuelekea michezo ya kufuzu michuano ya Euro 2024, Lakini mchezaji huyo ilithibitishwa na klabu yake kua alipata majeraha madogo yaliyomfanya kujitoa kwenye timu ya taifa ya Uingereza.
Marcus Rashford amekua kwenye kiwango bora sana msimu huu akiwa mfungaji bora ndani ya klabu hiyo mpaka sasa, Lakini mpaka sasa mshambuliaji huyo amekua kwenye mfungaji bora kwenye michuano ya Carabao Cup ambapo Man United wamemaliza kwa kutwa ubingwa huo.
Mshambuliaji Rashford amekua msaada mkubwa sana ndani ya klabu ya Manchester United msimu huu, akiwa kwenye ubora mkubwa sana hivo majeraha ambayo aliyapata karibuni yalifanya mashabiki wa klabu hiyo kuanza kuhofia lakini taarifa nzuri ni kua mchezaji huyo amerejea mazoezini.

