Kinda wa Brazil, Rodrygo amesema hataki kuwa “Neymar mpya” wakati akifafanua kulinganishwa kwake na nyota huyo wa Selecao.
Rodrygo ni mmoja wa wachezaji wachanga wenye vipaji katika mpira wa miguu akiwa na mabingwa wa La Liga, Real Madrid, akipata kutambuliwa kama mshindi wa Tuzo ya Goal NxGn 2020.

Winga huyo wa miaka 19 alihamia kwa Euro milioni 45 kutoka Santos kwenda Madrid mnamo 2019 na amekuwa akilinganishwa na mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Neymar na nyota wa Zamani wa Man City, Robinho, ambao wote walitokea katika klabu hiyo ya Brazil.
Amelinganishwa na Neymar tangu umri wa miaka 12, wakati aliposaini makubaliano na Nike kuwa mwanamichezo mdogo zaidi aliyewahi kudhaminiwa na kampuni hiyo.
Lakini Rodrygo hafurahii kulinganisha kwani yeye badala yake anatarajia kuunda njia yake mwenyewe, tofauti na hao wachezaji wengine.

“Tangu mwanzo wa taaluma yangu wakati naanza Santos, tayari walinilinganisha kama “Neymar mpya” na Robinho. Siku zote nilisema kwamba ninataka kuwa Rodrygo na kutengeneza historia yangu”.
“Robinho na Neymar ni wa kuigwa kiasi kikubwa kwa Santos na kwa maeneo yote ambayo walicheza, nadhani kuna Neymar mmoja tu”. alisema mchezaji huyo.
Naam, hapa ni mahali pako! Kuwa shujaa kwenye sloti hii ya Samurai Ken ujishindie mkwanja na kujipa burudani murua.



Caroline
Safi sana Rodrygo.tafuta njia yako.na sio kufananishwa na mtu
magdalena
kila mtu ana kiwango chake na uwezo wake awapo uwanjani kufananishana si jambo zuri
zeiyana
kiwango alichokua nacho Rodrygo cha kawaida tu hawezi kumfikia neyrma
Saupha mohamed
Hapana bado ajamfikia neyrma
Sauda
Anataka kuwa wa kipekee zaidi
Mwajumah
Hataki kufananishwa kwa sababu hawezi kuwa kama neyrma
Fatina mfigi
Kila m2 na kiwango chake awawezi kuwa saw
Adelta
Bado hawezi kumfikia Neymar
Antony Luseno
Nakala nzuri #meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri kilamtu anaupeo wake wakifikra kwaiyo yeye ataki kufananishwa na mtu
Ernest
Rodrygo amekuwa muwazi kuwa Neymar ni mchezaji wa kuigwa ila hataki kufananishwa nae,anataka kujijengea ufalme wake
felister
yupo sahihi anataka kua yeye kama yeye na sio kufananishwa
Janeflora malisa
Kwa kuwa sio kipofu lazim atembee anavyojua pongz sna Rodrygo
Tatu
Rodrygo yupo sahihi ataki kufananishwa na kitu chochote
Hopemwaikuka
Neymar ni mchezaj makin sana
Dorophina
Rodrygo hawezi kufikia kiwango hicho cha Neymar
Gabriel
hawezi kumfikia Neymar
Povel
Ni mapema kumfanishana neymar sema tumpe muda spoon hanawez kufik level ya neymar
Sabrina
Anajua Bado hajafikia kiwango cha Neymar
Elika
Hapo ni vitu viwili tofauti
Fatuma kasomo
Gud news
aisha
Nice
warda
Wivu tu