Salamu za Joan Laporta kwa Dembele

Joan Laporta ametuma ujumbe kwa Ousmane Dembélé huku kukiwa na kukwama kwa mazungumzo ya kandarasi.
Ousmane atamaliza mkataba wake na Barca msimu ujao wa joto, na jinsi mambo yalivyo, anaweza kuondoka klabuni hapo bure.

Barca wamedhamiria kukwepa suala la kuondoka bure, wana nia ya kumsainisha winga huyo kwa mkataba mpya mapema zaidi.

Lakini mazungumzo hayajaenda vizuri huku ripoti zikipendekeza kwamba, kwa jinsi mambo yalivyo, Dembélé ataondoka kweli msimu ujao wa joto.

Salamu za Joan Laporta kwa Dembele
Ousmane Dembele (Kushoto), Joan Laporta (Kulia)

Barca hawawezi kutoa mishahara ambao nyota huyu anahitaji anahitaji kwa sababu ya shida ya kifedha waliyonayo, lakini wakati huo huo, Laporta na mkufunzi mkuu Xavi Hernandez wanapendekeza Mfaransa kuwa ni sehemu muhimu ya mustakabali wa kilabu.

Laporta ametuma ujumbe kwa Dembélé wakati mazungumzo ya kandarasi yakiendelea kuzorota.

“Dembélé ni mchezaji muhimu sana, anaweza kutoa mengi zaidi kwa Barcelona kuliko alivyotoa. Ikiwa ataendelea na sisi, anaweza kufikia kuwa mchezaji wa kumbukumbu.”

Staa huyu amekuwa Barca tangu 2017 alipofikia kwa dili la thamani ya zaidi ya Euro milioni 130. Akiwa na miaka 24, bado kuna imani kwamba anaweza kufikia mafanikio makubwa akiwa Camp Nou.


MUDA WA KUJIACHIA NA CARNAVAL JACKPOT

Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.