Simba Yaendeleza Vichapo

Makala iliyopita
Mctominay Njia Nyeupe kueleka NapoliMakala ijayo
Chelsea Yatoa Kipigo kizito
Wekundu wa msimbazi walitawala zaidi kipindi cha kwanza cha mchezo huo kama ambavyo walifanya katika mchezo wao wa kwanza wa ligi kuu ya NBC dhidi ya Tabora United, Jambo ambalo liliwafanya vijana wa kocha Fadlu Davids kuweza kutengeneza nafasi nyingi za kufunga katika mchezo huo.
Klabu ya Simba haikuridhika na mabao matatu ambapo dakika ya 84 Valentino Mashaka ambaye alitokea nje alifanikiwa kupiga msumari wa mwisho katika mchezo huo akifunga bao la nne, Wekundu wa msimbazi sasa wanakwea kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya NBC wakiwa ana alama zao sita katika michezo miwili.