Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza Gareth Southgate ameonesha kuchukizwa na kitendo cha mshambuliaji wa klabu ya Manchester United Marcus Rashford baada ya kujiondoa kwenye timu hiyo.
Kauli ya kocha Gareth Southgate baada ya kupata ushindi dhidi ya timu ya taifa ya Italia siku ya ijumaa ilionesha wazi kocha huyo hajapendezwa na kitendo cha Rashford kujiondoa kwenye timu ya taifa ya Uingereza kuelekea michuano ya kufuzu mataifa ya Ulaya maarufu kama Euro.
Imekua kawaida kwa Marcus Rashford kujiondoa kwenye timu ya taifa ya Uingereza marta kwa mara pale ambapo anaitwa hasa kwenye michezo ya kufuzu au kirafiki na kusema amepatwa na majeraha, Kutokana na tabia hii imekua haimfurahishi kocha wa timu hiyo.
Baada ya mchezo dhidi ya timu ya taifa ya Italia kocha Southgate alisema hamna pengo lolote pale ambapo Marcus Rashford anakua hayupo kwenye timu hiyo, Kauli hii wengi wameitafsiri kama kocha huyo hapendezwi na tabia ya mchezaji huyo kutoka Manchester United.
Kauli ya kocha Southgate pia imekutana na mapingamizi kutoka kwa mashabiki wa klabu ya Manchester United mitandaoni ambao wanadai kocha huyo amekua hampi nafasi mchezaji huyo kwenye kikosi chake, Huku pia wakieleza kua mchezaji huyo ameshakwenda kwenye kambi ya timu ya taifa ya Uingereza mara kadhaa akiwa na majeraha hivo kocha huyo asimuandame mchezaji huyo.

