Steve Cooper ametangazwa kuwa mkufunzi mpya wa Nottingham Forest akichukua mikoba iliyoachwa na Chris Hughton.
Haughton alitupiwa virago wiki iliyoisha kutokana na mwanzo mbaya ambapo amepoteza mechi sita kati ya saba alizocheza msimu huu kwenye Championship.

Awali ilihusishwa kuwa John terry mlinzi wa zamani wa Chelsea kuwa ndio chaguo la kwanza baada ya kuachana na Aston Villa, lakini bodi imeamchagua Cooper kama chaguo la kwaza na wamekubali kuilipa Swansea na kumkaribisha kwenye dimba la City Ground.
Steve cooper mwenye umri wa miaka 41 ameliacha dimba la Liberty Stadium baada ya kuitumikia kwa misimu miwili.
Mkurugenzi wa Forest Dane murphy alinukiliwa “Steve alikuwa chaguo la kwanza kama mkufunzi mkuu, ‘tunafurahi kuweza kufanikishahilo, ‘uwezo wake wa kukuza vijana ni mzuri.”
“Kwa niaba ya mmiliki na bodi , tunakukaribisha na tunataraji kukupa msaada wowote utakao hitaji ili kwa mafimikio ya Nottingham Forest.” alimalizia Dane murphy
Ni wakati wa ushindi mkubwa ukiwa na kasino bomba ya Lock a Luck, meridianbet wanakupa sababu ya ushindi, funga bahati yako ya ushindi ukiwa na mabingwa.


