Ni suala la muda tu kabla benchi jipya la ufundi kuonekana kule Old Trafford. Mchongo utaanzia Carrington Training Complex, Ten Hag kuja na msaidizi wake kutoka Ajax.
Mitchell Van der Gaag natajwa kuwa kwenye mchakato wa kukamilisha vipengele vya mkataba wake na Man United ili aungane na Erik Ten Hag kuanzia msimu ujao. Haya ni mabadiliko mapya kwa Red Devils.

Kwa hali ilivyo mpaka sasa, mabadiliko ni makubwa kwenye bodi ya timu hiyo na, taarifa zinasema hili ni zoezi endelevu kuelekea ufunguzi rasmi ya dirisha kubwa la usajili mwezi ujao.
Van der Gaag anatajwa kama mtu muhimu kwenye mchakato wa kuijenga upya safu ya kuiongoza United na, mchakato wa kumsainisha United upo kwenye hatua za mwishoni kukamilika.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.