Mcheza Tenesi namba moja wa zamani kwa wanawake – Serena Williams amerejea kwa kishindo kunako michuano ya Top Seed Open.
Nguli huyo mwenye tuzo 23 za Grand Slam alijikuta akipambana kurudi mchezoni baada ya kuwa amezidiwa seti moja na mpinzani wake Bernarda Pera.

Katika mchezo huo, Bernarda alikuwa anaongoza kwa seti 4-6 0-4 na 4-4 katika seti ya pili ya michuano ya Top Seed Open inayochezwa jijini Kentucky – Marekani. Ndani ya saa 2 na dakika 15, Serena alipindua matokeo na kushinda kwa seti 4-4 6-4 6-1.
Serena amenukuliwa akisema ” Nilijua kama sitokata tamaa, nitacheza vizuri zaidi.”
Baada ya ushindi huu, Serena atakutana uso kwa uso na ndugu yake Venus Williams ambaye pia amewahi kuwa mchezaji namba moja duniani. Venus alimchakaza Victoria Azarenka kwa seti 6-3 6-2.

Mchezo wa mwisho katika ngazi ya mashindano ya Serena ulikuwa ni katika michuano ya Fed Cup Tie ambapo alichuana na Latvia mwezi Februari. Mchezo huo ulikuwa wa aina yake mapema kabisa baada ya Serena kukatisha mchezo wa kwanza na kugawa pointi kwa mpinzani wake katika mchezo wa pili.
Katika mchezo wa tisa, mambo yalibadilika na kuanza kumnyookea Serena ambaye aliibuka kidedea mwishoni mwa mchezo huo.

Serena anapanga kushiriki michuano yote ya US Open inayochezwa mwezi huu, pamoja na French Open iliyopangwa kuchezwa mwezi Septemba baada ya Mlipuko wa Virusi vya Corona.
Hii ni michuano ya kwanza kwa wanawake tangu kifo cha George Floyd kilichozua gumzo na maandamano katika sehemu mbalimbali za ulimwengu kupinga ubaguzi wa rangi. Michuano hii inaendelea kusimamia msemo wa “Black Lives Matter” katika michezo yote.
Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Basi fahamu kuwa kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.


Dorophina
Serena talent player
Khadija
safi sana serena#meridianbettz
Sauda
Serena fundi
Zeiyana
Serena ndio nguli wa tenesi
rama
Maoni:serena ndo atakuwa bingwa wa michuano hiyoo
Fatina mfingi
Serena moto wa kuotea mbali
aisha
Big up kwa serena uko vizuri dada
Adelta
Serena Ni fundi
@meridianbettz
Caroline
Serena William ndo bingwa wa Tennis
Mwajumah
Serena ndio fundi wa tenesi anajua sana uyu dada#Meridianbettz
Ester jackson
Katika wachezaji wa tenes Serena William ndio namba moja ambaye namkubali sana hata ukiangalia historia yake tangu yupo mdogo anajua sana aliweza kumshinda Dada yake akiwa mdogo hivyo ananipelekea kuwa anashinda mbele ya shindano ambalo atacheza na Dada yake.
Tatu
Serena yupo vizuri
Sabrina
Namuaminia sana Serena kwenye tenes
felister
serena hana mpinzani kwa upande wa tenisi
Sadick
Serena ni mmoja wa wachezaji tennis ambaye amekuwa na kiwango cha juu tangu aanze kucheza#meridianbettz
Theonestina
Serena yuko vizur Sana
farida ahmadi
Yuko vizuri Sana Serena
Latifa juma mohamed
Among the talent player
Samiah
Serena yupo vzr
Nasra
Serena yupo vzuri
Lydia Emmanuel Magoti
Safii Sana Selena namuelewa Sana mdada anaejiweza kupambana kwenye tenes namkubali
Furahav
Serena namkubali sana.
Gabriel
Nimefurah kumuona Serena William anarud kwa kasi maana alipotea sana pia alishuka sana kiwango na kuanza kufungwa na vijana wanaochipukia but I’m enjoyed
magdalena
serena amekuwa akifanya vyema sana katika huu mchezo na ataendelea kufanya maajabu zaidi habar njema kwa mashabiki wake
David Pere
Nimefurah kumuona Serena William anarud kwa kasi maana alipotea sana pia alishuka sana kiwango na kuanza kufungwa na vijana wanaochipukia
warda
Serena Huwa Yupo Juu sana