Ripoti zinataja Tottenham wanafanyia kazi angalau saini tano zaidi baada ya kumaliza kumnasa Pierre-Emile Hojbjerg kutoka Southampton.
Wana London hawa walitangaza kuwasili kwa Hojberg jana kwa ada ya £15millioni ambayo kuna uwezekano wa kuongezeka hadi pauni 19m.
Taarifa kutoka chanzo cha ndani ya klabu kinasema kuwa Spurs wanajiandaa kusajili wachezaji wengine 5 wapya wakati Jose Mourinho akijaribu kuboresha kikosi kabla ya kampeni mpya.
Mreno huyu anajaribu kusaini beki wa kulia, beki wa katikati, kiungo mshambuliaji, mshambuliaji anayeweza kufanya kazi popote kwenye safu ya ushambuliaji na kipa wa ziada.
Mourinho anatajwa kuwa tayari ameshaweka vipaumbele vyake tayari, na hilo ndiyo jema zaidi kwake, baada ya kutua Hojbjerg ambaye walikuwa wakimlenga kwa mda mrefu.
Lazima Tottenham Wauze ili Wanunue
Ili kufanya ununuzi mkubwa Tottenham wanapaswa kuuza. Wana hawa wa London wako kwenye mazungumzo ya kumuuza Serge Aurier, mchezaji anayetumai anaweza kuipa klabu angalau £20m baada ya £12m ya Kyle Walker-Peters.
Nyota wengine wanaotarajiwa kuondoka Tottenham wanaweza kuwa ni pamoja na mabeki Juan Foyth, Danny Rose na Cameron Carter-Vickers pamoja na kiungo mshambuliaji wa muda mrefu Erik Lamela.
Kuna uvumi kwamba Tanguy Ndombele pia ataondoka Spurs, ikiwa ni pamoja na uwezekano wa kuhusika kwenye mpango wa kubadilishana wachezaji ambao unaweza kuwaleta nyota kadhaa wakubwa pale Spurs.
Hata hivyo, klabu ya Tottenham imekuwa ikipuuza taarifa hizi na kutotaka kuzungumzia sana.
Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.


Leonard
Vizuri kama wakiboresha kikosi chao ili waje walete ushindani
Ester jackson
Of a hivyo sasa kwa timu zisizo na mabeki kama Chelsea ni muda wenu sasa
Shan
Safi!
felister
sio mbaya ili kuboresha kikosi msimu mpya
Sauda
Ni vizuri ili kuimarisha kikosi msimu ujao
Shafii
Spurs wanataka kutengeneza kikosi cha ushindani msimu ujao ni jambo zuri kwa wana spurs.
Caroline
Tunasubiri kuona wachezaji watakaosajiliwa
Nasra
Morinho anampango wa kutengeneza kikosi Cha Spurs ambacho kitakuja kuleta ushindani msimu ujao ni Jambo la furaha Sana kwa Wana Spurs.
Zeiyana
Tottenham wanajipanga kikamirifu ligi msimu hujao
Dorophina
Msimu ujao Tottenham lazima watakuwa fiti sana
Sadick
Tottenham imeshiriki ligi ya mabingwa kwa misimu minne iliyopita na msimu ujao itakosa nafasi hiyo pengine usajiri mzuri utapelekea kurudi katika nafsi yake ya juu kwenye ligi ya EPL#meridianbettz
Devotha
Tunasubiri maajabu ya usajili huo msimu ujao
Khadija
Tunasubili tuone maajabu huo msimu ujao usajili utakuwaje#meridianbettz
Povel
Kila la kheri Ila vigezo na masharti wazingatieh wasije wakakutwa na rungu la UEFA
aisha
Ni vizuri kuboresha kikosi chao ili walete mabadiliko katika club yao
Fatuma kasomo
Msimu ujao nijambo zuri wana spurs
Shan
Imekaa poa tusubir tuone!!
Tatu
Muda wa kusajili viungo na kujipanga kikosi
Gabriel
Habar njema
Sabrina
Basi sawa
Theonestina
Habari njema Sana
Hope mwaikuka
We are waiting for this
Mariam mtandama
Habari njema
Rose kapinga
Safiiii tunasubir mabadiliko!!!!
Rehema
Iko vizur
Adelta
Ni vizuri kuimarisha kikosi
@meridianbettz
Fatina mfingi
Tunasubir mabadiliko ss mashabiki
Njiku
Hii ipo poa sana kwa tottenham na kocha wao kibuli
Ernest
Sasa ni wakati wa Mourinho kufanya yake kwenye usajiri
Salma ngende
Kikosi kitakuwa safi
Saupha mohamed
Aya sasa aweke sawa kikosi chake
Furahav
Tunasubili tuone.
magdalena
apo kocha wa spurs akiweka daau zuri zaidi atasajili wachezaji wazuri zaidi
David Pere
Kocha wa kukutupuka kashaanza kazi yake
warda
Wasuke suke tu watapata wachezaji wazuri