Tetesi zinasema Barcelona huenda ikamsajili mshambuliaji wa Liverpool raia wa Senegal Sadio Mane, 28, au kiungo wa kati wa Uholanzi Gini Wijnaldum, 30, baada ya kipengee katika makubaliano yaliyowezesha Philippe Coutinho kwenda Nou Camp kumalizika.
Mgombea urais wa Barcelona Emili Rousaud anasema ikiwa atachaguliwa atasajili “wachezaji wawili wazuri, mmoja wao akiwa Neymar”, mshambuliaji wa Brazil, 28, ambaye aliweka rekodi ya dunia ya uhamisho kutoka Barca hadi Paris St Germain mwaka 2017.
Tetesi zinasema Manchester United bado haijakata tamaa ya kumsajili mchezaji wa Barcelona Ousmane Dembele lakini itajitahidi kufikia makubaliano ya mkopo kwa mshambuliaji huyo wa Ufaransa, 23.
Mkurugenzi wa Borussia Dortmund Michael Zorc anaona mshambuliaji wa Norway Erling Braut Haaland ataendelea kusalia katika klabu hiyo “kwa muda mrefu” licha ya mchezaji huyo, 20, kuhusishwa na kuhamia Real Madrid.
Tetesi zinasema Chelsea inamnyatia beki wa kati wa Atletico Madrid na Uruguay Jose Gimenez, 25.
Tetesi zinasema Tottenham iko tayari kumsajili winga wa Leicester Demarai Gray, 24, kwa uhamisho wa bila malipo Januari.
Liverpool huenda ikapata kima cha pauni milioni 30 dirisha la usajili litakapofunguliwa Januari kwa kumuuza kiungo wa kati wa Uswisi Xherdan Shaqiri, 29, na mshambuiaji wa Ubelgiji Divock Origi, 25.
Tetesi zinasema mlinda lango wa Italia Gianluigi Donnarumma, 21, anakaribia kukubali mkataba mpya na AC Milan.
Manchester United imetoa ofa mpya kwa mchezaji Timothy Fosu-Mensah,22, wa Uholanzi anayeweza kucheza nafasi kadhaa ambaye mkataba wake unamalizika msimu ujao.
Tetesi zinasema West Brom inamfuatilia kiungo wa kati wa Celtic raia wa Ufaransa Ntcham, 24.
Aston Villa huenda ikatenga kitita cha pesa Januari kwa ajili ya winga wa Werder Bremen raia wa Kosovo Milot Rashica, 24, ambaye pia amehusishwa na RB Leipzig, Bayer Leverkusen na Wolfsburg.
Mchezaji wa QPR Bright Osayi-Samuel ameambiwa aache kuwa na wasiwasi huku winga huyo mzaliwa wa Nigeria, 22, akihusishwa na Burnley, Celtic, Fulham, Leeds United na Leicester.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.
Caroline
Asante kwa taarifa
Fatina mfingi
Duuh fanyan mumchukue mane yuko vizur sanaa
Lydia Emmanuel Magoti
Itakuwa vizuri wakimsajili kiungo huyo mane
Shakila mrope
Itakuwa vizuri mkimchukuwa
Adelta
Kiungo huyo Yuko makini wamsajili tu
Tatu
Wamchukue tu mane
samiah
Duuh
Fatuma kasomo
Noma
Magdalena
Barcelona wakimsajili uyo jamaa watakuwa wamepata kijana makini
Saupha mohamed
Good news
aisha
Kama itakua kweli barc watatisha sana
Dorophina
Barca wakifanikiwa kumsajili mane itakuwa poa sana watakuwa wamepata mchezaji bora sana
Hopemwaikuka
Mtanifurahisha sana
Rahma
Hatali
Sauda
Makala bomba
Sabrina
Taarifa ziko vizuri
warda
Itakuwa poa sana