Tetesi za Soka Barani Ulaya.


Tetesi zinasema Liverpool wanapanga uhamisho wa mkopo kwa mchezaji wa nafasi ya ulinzi wa New York Red Bulls Aaron Long, 28. Klabu hiyo ya Anfield inajiandaa kutumia saa 72 za mwisho za dirisha la usajili, kumsajili mlinzi wa kati baada ya Joel Matip kuwa majeruhi.

Tetesi zinasema Real Madrdid watatupa karata yao kwa mshambuliaji wa Ufaransa na Paris St-Germain Kylian Mbappe, 22, msimu huu.

Tetesi zinasema Paris St-Germain wana nia ya kuwaunganisha tena kocha Mauricio Pochettino na kiungo wa Tottenham Dele Alli, 24.

 

Dele Alli Kwenda PSG

Tetesi zinasema winga wa England na klabu ya Leicester City , Demarai Gray, 24, ameridhia masharti binafsi na Bayer Leverkusen lakini klabu hizo mbili vinavutana kuhusu ada.

Mchezaji wa nafasi ya ulinzi Sergio Ramos, 34, bado hajakubali mkataba mpya na Real Madrid, mwezi mmoja baada ya pande hizo mbili kukutana kujadiliana kuhusu kuongeza mkataba wake, ambao utakwisha msimu huu.

Timu ya Uturuki ya Trabzonspor inaamini imefikia makubaliano ya kumsajili beki wa kushoto wa Tottenham Danny Rose, 30.

Tetesi zinasema Manchester City wanakaribia kuwasajili makinda mawili wa Fluminense na raia wa Brazil Kayky na Metinho, wote wenye umri wa miaka 17, kwa kitita cha pauni milioni 9.

Southampton na Westbrom wanajaribu kumsajili kiungo wa kati wa Arsenal Ansley Maitlan-Niles,23, kwa mkopo kabla ya dirisha la usajili la mwezi Januari kufungwa Jumatatu.

Klabu hiyo ya Pep Guardiola haina mpango na mchezaji wa nafasi ya ulinzi wa Bayern Munich David Alaba, 28, kwa kuwa klabu inampango wa kumsajili mchezaji wa nafasi ya ushambuliaji.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Tetesi zinasema kocha wa zamani wa Chelsea na Tottenham Andre Villas-Boas, 43, anatarajiwa kuondoka Marseille mwishoni mwa msimu.

Mshambuliaji wa Wolves Patrick Cutrone, 23, anajiandaa kujiunga kwa mkopo na klabu ya Valencia kwa msimu wote uliosalia baada ya uhamisho wake kwa mkopo katika klabu ya Fiorentina kumalizika mapema.

West Brom wamekubali kumsajili kiungo wa kati wa Celta Vigo,Okay Yokuslu, 26, ingawa wanahitaji kumshawishi mchezaji huyo.

Tetesi zinasema mchezaji wa Aston Villa, Mfaransa Frederic Guilbert, 26, amekubali uhamisho wa mkopo kuelekea Strasbourg.

Tetesi zinasema Mshambuliaji wa Everton Cenk Tosun, 29, anataka kurejea kwenye klabu yake ya zamani ya Besiktas kwa mkopo.

Mlinda mlango wa Denmark Jonas Lossl,31, ataondoka Everton na kusajiliwa na klabu yake ya zamani ya FC Midtjylland.


MSHINDANI HUSHINDA BWANA!

Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!

Fairy-in-Wonderland_Casino-Post_25-January

CHEZA SASA

11 Komentara

    Tetesi zinasomeka

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Tetesi zimetulia

    Jibu

    Makala imetulia

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Naona dirisha dogo la usajili Mambo yanazidi kupamba Moto

    Jibu

    Tetesi safi

    Jibu

    Tetesi zipo poa

    Jibu

    Liverpool watafanikiwa kumsajili mchezaji huyo kwa masaa yaliyobaki

    Jibu

    Hasante meridian kwa makara nzuli

    Jibu

    Safi

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.