Tetesi zinasema, Mshambuliaji wa Manchester United na Ureno Cristiano Ronaldo, 37, amefanya mazungumzo na wakala wake Jorge Mendes kuhusu hatma yake Old Trafford.
Tetesi zinasema, Mshambuliaji wa Bayern Munich na Poland wa miaka 33- Robert Lewandowski ananyatiwa na Manchester United.
Tetesi zinasema, Meneja wa Aston Villa Steven Gerrard anataka klabu hiyo kutekeleza chaguo lao la kumsajili Philippe Coutinho kwa euro 40m (£33.5m).

Kocha wa Chelsea Thomas Tuchel ametoa wito kwa mlinzi wa Denmark Andreas Christensen, 25, kupuuza tetesi za kujiunga na Barcelona na kubakia Stamford Bridge.
Arsenal wameweka kipaumbele kuwasajili washambuliaji wawili na kiungo wa kati mmoja kama sehemu ya kuimarisha kikosi chao msimu huu wa joto.
Sevilla wameongeza kipengele cha kuuzwa kwa Diego Carlos hadi euro milioni 80 (£67m). Newcastle ilijaribu kumsajili Mbrazil huyo mwenye umri wa miaka 28 mwezi Januari lakini timu hiyo ya Uhispania haikuwa tayari kumuuza beki huyo.

Atletico Madrid wanaongoza katika mbio za kumsajili kiungo mahiri wa Ufaransa na Marseille Boubacar Kamara. Manchester United na Newcastle pia wamehusishwa na uhamiso wa mchezaji huyo wa miaka 22.
Winga wa Uhispania Bryan Gil, 21, anaweza kusalia Valencia msimu ujao baada ya kujiunga na klabu hiyo kwa mkopo Tottenham mwezi Januari.
Tetesi zinasema, Kiungo wa Uholanzo Ryan Gravenberch, 19, yuko tayari kujiunga na Barcelona kutoka Ajax msimu huu wa joto.
Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000 katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.


