MJUMBE wa Kamati ya Usajili wa Yanga na Mkurugenzi Uwekezaji wa GSM, Injinia Hersi Said, amesema hawakuwa na mpango kabisa wa kumsajili kiungo mchezeshaji mpya Simba raia wa Zambia, Larry Bwalya huku akisisitiza yeye alimuulizia Clatous Chama kwa meneja wake.
Hivi karibuni kuliibuka tetesi za Yanga kuwepo kwenye mipango ya kumsajili Bwalya kabla ya siku chache Simba kuchukua maamuzi ya haraka kufanikisha saini ya nyota huyo.Kiungo huyo amesajiliwa na Simba kwa mkataba wa miaka miwili kukipiga hapo akitokea Power Dynamos inayoshiriki Ligi Kuu ya Zambia kama mchezaji huru baada ya mkataba wake kumalizika huko.

Akizungumza jijini Dar jana, Hersi alisema kuwa meneja wa Chama ndiye anayemsimamia Bwalya ambaye yeye alifanya mawasiliano naye kumuuliza kama kuna uwezekano wa kumpata Chama.

“Meneja wa Chama ndiye huyo wa Bwalya, mimi nilichofanya kumuulizia Chama nikionyesha nia ya kumsajili, lakini sasa kilichotokea ni meneja huyo kuwapigia simu viongozi wa Simba kwa ajili ya kuwajaza.

“Meneja huyo aliwapigia simu Simba kwa kuwaambia kuwa, Yanga wameonyesha nia ya kumsajili Bwalya kwa lengo la kuwaongezea kasi viongozi hao ili kukamilisha dili hilo la usajili haraka.
“Huyo Bwalya hatukuwa katika mipango naye kabisa, Chama kweli lakini siyo huyo kiungo, nikuhakikishie kuwa Yanga tukihitaji jambo letu hivi hakuna wa kulizuia kama tulivyoamua kwa Mwamnyeto (Bakari) kumsajili.
Beti Mbio za Mbwa Mubashara
Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.


Dorophina
Hersi yupo sahihi yanga nia yao ilikuwa ni chama na sio mchezaji mwingine tatizo simba wanapata tabu sana kuambiwa kwamba yanga wanamtaka bwalya wakamuwahi wao kumbe sio tegemeo la yanga chama angesajiliwa na yanga ingekuwa poa sana
rama
mhhh yanga singe weza kuwapata wachezaji hao bhana
Devotha
Asante kwa taarifa
Mwajumah
Mh yanga mnatapatapa sana mnapesa ya kumnunua chama nyie#Meridianbettz
felister
yanga tukiamua jambo letu hakuna wa kutuzuia#Mwajumah
Fatina mfingi
Mmh yanga hamna jipya
Caroline
Lakini sio mbaya.kikosi kipo vizuri.wasubiri Mambo mazuri kutoka yanga
Ernest
Maneno mengi ya nini leo ndio tutaanza kuona jambo la wananchi pale kwa Mkapa
Tatu
Tatizo yanga wanamaneno mengi
Povel
Duh noma sana hiiii
Latifa juma mohamed
Asanteni kwa taarifa
Fatuma kasomo
Maneno mengi yanini
Lydia Emmanuel Magoti
Chama niwasimba tuuu akuna chama watimu nyingine atabaki kuwa Simba sio krabu nyingine
Agness
Yanga hamna kitu
Sadick
Ikiwa kweli alimuhitaji Chama nadhani alitakiwa kuongea na Simba ambayo Chama anachezea kwa sasa,tatizo timu zetu zimekuwa zikikurupuka na kuvamia mambo mwisho wa siku zinaishia kwenye migogoro inayoweza kuepukika#meridianbettz
Nasra
Yanga mpya naiona
Antony Luseno
Roho ya simba fc ni chama kwa sasa sidhani kama wangemwachia
aisha
Yanga hamna maajabu kila siku maneno nyie jamani
Amiri Kayera
He kumbe!
farida ahmadi
Asante kwa kunijuza
Rehema
Aisee noma sana
Rose kapinga
Yanga mbwembwe nying,tunataka vitendo!!!
Furahav
Chama yuko vizuri sana.
Hope mwaikuka
Maneno ya mkosaji hayo
Amani
Simba wasinge weza kumuuza pia yanga Awana ela ya kumnunua
Neema
Yangaa badoo sijawakatia tamaa
Sabrina
Yanga muwaache wafanye yao
lombo
mambo ni moto na meridianbet
Samiah
Dakika 90 ndio zitaongea
Zeiyana
Yanga bado wanakikosi kizuri tu
Saupha mohamed
Yanga Anna kitu
Asia Abdy
Yanga haina shuhul
Issa
Hana jambo jipya
Janeflora malisa
Mambo meus hapa hakun maajabu
Ester jackson
Kumsajil mchezaji sio tatinzo tatizo lipo kwa makala wao na timu zetu zinawasiliano mazuri lakini hakuna kabisa hawawezi wakupe bati wakati nyumba yao yavuja huu utakuwa uzembe
Sauda
Chama akiwa Yanga ni raha tupu
warda
Hatuwezi kumwachia kabisa Chama
Johnmary joel
Habari njema#meridianbett
magdalena
yanga wapambane wawezavyo ila chama kumpata sio rahisi watafute tu mtu mwingine watuachie chama wetu sisi wana simba tena watulie kabla hatujawafokea
Shafii
Kumbe bwalya hakua kabisa kwenye mipango ya yanga.
David Pere
Ikiwa kweli alimuhitaji Chama nadhani alitakiwa kuongea na Simba ambayo Chama anachezea kwa sasa,tatizo timu zetu zimekuwa zikikurupuka na kuvamia mambo mwisho wa siku zinaishia kwenye migogoro inayoweza kuepukik
Gabriel
Yanga wako vzur hawahitaji mchezaji yoyote kikosi Kiko vzur huyo chama tokea akutwe na irizi hana maajabu