“Uamuzi wa Mwisho ni 2021 Kuchezwa Olympics!” – Thomas Bach

Kiongozi mkuu wa michuano ya Olympics, Thomas Bach amesema kuwa mwaka 2021 ni uamuzi wao wa mwisho juu ya ni lini michuano hiyo itafanyika tena ikiwa ni baada ya michuano hiyo iliyopangwa kufanyikia Tokyo kusogezwa mbele.

Ameyasema hayo siku ya Alhamisi akikazia suala la kwamba haiwezekani michuano ile ikasogezwa mbele zaidi ya ilivyo sasa.

Wakati Bach akizungumza na BBC aliwaambia kuwa amekubaliana na maoni ya Japan kuwa gemu hizo zitatakiwa kusimama kwa muda kutokana na janga la Corona na itatakiwa kuendelea endapo ugonjwa usipopatiwa ufumbuzi hadi kufikia mwakani.

Mwezi Machi, michuano ya Tokyo 2020 Olympics iliahirishwa mpaka ifikapo Julai 23, 2021 wakati maambukizi ya ugonjwa wa Corona yakiwa yamepamba moto kwa sasa duniani na kupelekea michezo mingi kusimama kabisa.

“Ni sahihi kwamba ninaelewa hali ya Japan kwa sasa lakini huwezi kuacha hali hii ikaendelea milele,” rais huyo wa International Olympic Committee alisema.

“Huwezi kubadili michezo yote kwa mwaka mzima duniani kote kwa mashindano yote makubwa.

“Hauwezi kuwaweka katika sintofahamu wachezaji wote wanaohusika, hauwezi kuruhusu hali hii ikaendelea milele hasa katika michuano ya Olympic.”

Michuano ya Olympics haijawahi kufutwa ukiachana na nyakati zile za kutokea kwa vita za kidunia lakini Wajapan na viongozi wao wamesema kwamba kwa sasa hawana lengo la kuendelea kuahirisha zaidi michezo hiyo zaidi ya hapo mwakani.

31 Komentara

    ni swala la kumuomba MUNGU tu hali ikae sawa Olympic sio bora zaidi ya Uhai wa watu bhana

    Jibu

    Ni lazima wakubali Hali halisi ilivyo kwa sasa

    Jibu

    Corona imeasili vitu vingi Sana duniani.mungu atunusuru kwakwer

    Jibu

    Mmh asante kwa taarifa #meridianbet

    Jibu

    Ni Jambo la kuwah nasubir tu mpka Hali itakapo kuwah sawa kwn ni janga la dunia

    Jibu

    gud newz asante

    Jibu

    kila kitu kitakaa sawa kusogezwa mbele sio mwisho

    Jibu

    Tuombe mungu mambo yakae sawa

    Jibu

    Wakubaliane na hari ilivyo sasa

    Jibu

    Tuombe Mungu na kuchukua taadhari hakika kila kitu kitakuwa sawa

    Jibu

    Tnx 4 news# meridianBetTZ

    Jibu

    Kikubwaa ni kumuombaa Mungu na kuchukuwa tahadhari

    Jibu

    Uvumilivu nijambo zuri,maana kwa ugonjwa huu wa corona sio poa kabisa

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    sidhani kama wajapan wamefurahi maana walikuwa walazimisha sana michezo iendelee

    Jibu

    Safi Sana maana kila kitu kina nafasi yake kwenye maisha

    Jibu

    Ni sawa ni kuomba uzima tuu .

    Jibu

    Ahsant sana meridianbet kwa habari njema

    Jibu

    Hili gonjwa liishe tu

    Jibu

    Habari nzur

    Jibu

    ni kumuomba mungu tu ili gonjwa litokomee mana ni la balaa

    Jibu

    Maamuzi mazuri yamefanywa na kamati hii

    Jibu

    Maamuzi mazuri yamefanywa na kiongozi huyo

    Jibu

    Ni katika kujilinda na covid19

    Jibu

    Corona kajua kutuaribia mambo#Meridianbettz

    Jibu

    Ni uamuzi sahihi japokuwa unaweza kutenguliwa muda wowote.

    Jibu

    ahsanteni meridianbet kwa habari motomoto

    Jibu

    Meridian mnanipa furaha kwa taarifa motomoto#meridianbettz

    Jibu

    Tumuombe Mungu uzima tufike salama hiyo 2021

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Olimpik ni michezo mizuri

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.