Ukimsema Ajibu, Mtazame Mkude

Wengi tumekuwa tukimtupia lawama Ibrahimu Ajibu kushindwa kutambua thamani ya kipaji chake angalau aionje pepo ya soka la kulipwa huko ng’ambo.

Ni mwendawazimu tu atakidharau kipaji maridhawa alichonacho Ajibu ila akisema neno katika utunzaji wake , nia ya kufika mbali basi hapo anaweza kuwa ameianza safari ya kueleweka na wadau wote wa soka nchini.

Wakati jana nautazama mpira wa watani wa jadi hususani idara ya kiungo ya Simba SC iliyokuwa chini ya mkongwe Jonasi Mkude , nilitafakari mambo mengi sana . Moja ya tafakuri yangu ilikuwa kwa wale ambao wanaomnyooshea kidole Ajibu , wapo wapi au tangu huyu mwamba anaibuka na sasa anaianza safari yake ya magharibi ya soka hawajamuona?

Jonas Mkude naweza sema ni mmoja wa viungo hatari nchi hii ambao wanaijua vyema kazi ya kiungo mkabaji na variations zake zote. Ni miaka takribani 10 thamani ya kiungo huyu haijawahi kushuka wala kutetereka nchi hii.

Unaweza kukaa na kujiuliza nini kimempata classic player kama huyu kushindwa kuvuka mpaka wa nchi yetu kwenda ng’ambo kuongeza thamani ya soka lake .

Katika vikosi vyote vya jana kwa Simba na Yanga , Mkude ndio alikuwa mchezaji pekee ambaye amecheza mechi nyingi za watani wa jadi, hivyo alikuwa na uzoefu wa kutosha kabla ya Yondani kuingia kipindi cha pili ambaye ndio mchezaji anayeshikiria rekodi kwa sasa Tanzania kucheza mechi nyingi zaidi za watani wa jadi .

Mkude kumalizia soka lake nchini ni mwendelezo wa soka letu kwa ujumla kushindwa kuwatoa nje wachezaji wenye vipaji vizuri kwenda kuongeza thamani ya vipaji vyao.

Ni wakati sasa kwa wachezaji chipukizi pamoja na viongozi wao kuinua macho yao ili waweze kutazama mbali zaidi kuliko kuridhika na malisho haya ya nyumbani. Wengi tulimshuhudia Feisal jana akiwa bora katikati ya kikosi kibovu cha Yanga kilichokubali kichapo cha 4-1 kutoka kwa Simba.

Feisal ni hazina kwa taifa endapo katika umri huu mdogo atapata njia sahihi ya kwenda mbali kisoka . Licha ya kufika EPL , Samatta amekaririwa akisema anatamani angefika katika ligi hiyo kubwa duniani akiwa na umri mdogo . Hii inaonesha ni vyema kuyaandaa mafanikio yako angali bado una nguvu na damu inachemka.


Kuna ofa kibao sana unzaofaidi ikiwa unabashiri na Meridianbet. Jiunge sasa kufurahia ofa zetu.

Bonyeza HAPA Kujiunga.

39 Komentara

    Ukizungumzia kikosi cha simba ukosi kumuonge4a jonas mkude ni kiungo machachari tatizo nyota kinachomfanya akose kucheza clabu za nja

    Jibu

    Mmh asanteni kwa taarifaa

    Jibu

    Hapa huwa napata shida kujua kama ni wachexzaji wenyewe ndio hawataki kuvuka mipaka au kuna kitu nyuma ya pazia

    Jibu

    Uenda wakawa wanatamani kutoka nje lakini hawajapata connection yoyote ya kuwatoa nje

    Jibu

    Tnx meridian kwa update za kimichezo

    Jibu

    Huenda wachezaji wenyew ndio hawataki kuvuka boda

    Jibu

    Good news

    Jibu

    jonasi mkude ni moja wa kiungo mahiri sana

    Jibu

    Asante

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Ahsant meridian kwa taarifa

    Jibu

    Kweli kabsa vizuri kundaa matarajio yako ya mbele bado una umri mdogo

    Jibu

    Mkude nikiungo mzuri Sana mpambanaji Sana yani atakama anakasolo zake zaujeuli nikawaida sisi binadamu atuja kamilika lakini mkude yeye binafsi yake anajua kulitumikia soka na hanajua nn anakifanya mpambanaji huyo ajawai kushuka kisoka kiungo mshambuliaji bek huyo anajua

    Jibu

    Wachezaji wengi hawana mitazamo ya mbali wanaona kufika simba ama yanga ndio wamemaliza

    Jibu

    mchezaji mwenyewe mawazo ayo hana akichezea yanga au Simba anaona kashafika

    Jibu

    Tatizo wachezaji wetu wanacheza na majini mfukoni,waonekana wazuri kumbe wanamajini mfukoni,wakitoka nje wanakuwa hakuna kitu.

    Jibu

    Naona tatizo connection

    Jibu

    Makala safi

    Jibu

    Wachezaji wetu wanataka kucheza simba au yanga ndio mitazamo yao

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Ajibu talent player#meridianbettz

    Jibu

    Lakini bado hajitambui Ndio maana anabakia kuwa mchezaji wa ridhaa tu mpaka mwisho wa soka lake

    Jibu

    Feisali bado kijana mdogo sana lakini hanaonesha hana uwezo mkubwa sana lakini hajapata timu ya kuichezea ushauri wangu hasikate tamaa kwani kufanikiwa kunatakiwa kujitoa sana..!big up sana dogo kazi yako inaonekana

    Jibu

    Kwer kbx

    Jibu

    Kila ktu kina mda wake

    Jibu

    Bonge la makala

    Jibu

    Kawaida sana

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Makala iko vizuri.

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

    Kweli mnatupa ufafanuzi akinifu kabisa,ndani Ajibu pembeni Mkude

    Jibu

    Nihabari njema

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Makala nzuri sana hii

    Jibu

    Habari nzuri Sana

    Jibu

    asante kwa makala

    Jibu

    Asanteni meridianbet kwa makala nzuri

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.