Kama walivyokuwa njiani kuonesha nia yao ya kumsajili nyota wa Swansea City baada ya kuridhishwa na mchezaji huyo kwa kadri ya mahitaji ya kocha wa kikosi hicho, klabu hiyo kwa sasa imefanikisha kunasa saini ya nyota James ili aweze kuhudumu katika kikosi hicho ambacho kwa sasa kinaamini sana katika kukuza matumizi ya vijana.
Klabu hiyo kwa sasa imefikia hatua zake za mwisho kabisa kukamilisha dili la kumnasa kinda huyo ili aweze kutimiza mahitaji ya klabu kujenga kikosi chao ambacho kimepoteana sana. Kwa sasa wapo kwenye mipango kabambe ya kurejesha heshima.
Wakongwe wa klabu hiyo akiwemo Giggs wamshauri kijana huyo kukubaliana na ushindani wa klabu hiyo maana sio sehemu ya kupumzika na wanapaswa kuwekeza ushindani wa aina yake kutoka kwenye nafasi ambazo klabu imewekeza nguvu kubwa kwao.
Inakumbukwa kwamba mchezaji huyo yupo chini ya utawala wa Giggs kwa msimu ambao kocha huyo anahudumu kama kocha mkuu wa klabu hiyo ila kwa sasa amemuita katika timu hiyo ya taifa kwa maana hiyo anajua nje na ndani za kijana huyo na anapaswa kuweka nguvu za kutosha.
£18m ndizo zinazomtoa nyota huyo kutoka kikosini hapo kuelekea kwa miamba hao wa soka nchini Uingereza wakiwa na mataji mengi ya kihistoria. Na sasa wanarudi tena kwa awamu nyingine wakiwa na upinzani ambao utaleta hamasa katika ligi hiyo chini ya Ole.
James ana msimu mmoja ndani ya klabu ya wakubwa na ameweza kuvuta jicho la klabu na timu ya taifa pia. Mkongwe wa klabu hiyo, Giggs anaamini kabisa kwamba kwa namna anavyomfahamu nyota huyo ni biashara yenye manufaa sana kwa klabu hiyo na ataisaidia sana.
Mashabiki wengi bado hawajajenga imani kwa mchezaji huyo kuwa na msaada mkubwa sana ndani ya kikosi hicho. Japo suala hilo ni gumu sana kuliamini kwa haraka hadi watakapoona nini kinafanywa na mchezaji huyo ndani ya uwanja. Wao wanachokiamini ni kupata wachezaji wenye majina makubwa.
Kikubwa ambacho kila mmoja anakisubiri ni aina ya mafanikio ambayo nyota huyo atayashusha ndani ya klabu hiyo ikiwa kama sehemu ya maendeleo ya klabu. Kama akiweza kuonesha ushindani ni sehemu ambayo itakuwa salama sana kwake maana klabu hiyo ni kama daraja la mafanikio kwake.
Asia Abdy
Tunategemea mafanikio kwenye klabu kama watafanikiwa