Waziri Mkuu Ataka Fainali ya UCL, Uingereza

Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson amelitaka shirikisho la soka barani Ulaya ‘Uefa’ kuhamishia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwenda Uingereza ili kutoa nafasi ya mashabiki kwenda kuishuhudia uwanjani.

waziri mkuu

Mchezo huo umepangwa kufanyika kwenye nchi ya Uturuki ambayo imewekwa kwenye mstari mwekundu na Uingereza kama nchi yenye maambukizi ya virusi vya corona, hivyo mashabiki wa Chelsea na Manchester City watakaokwenda kushuhudia fainali hiyo watalamizika kuingia gharama nyingine za kujitenga hotelini kwa siku 10 watakaporejea kutoka Istanbul baada ya fainali hiyo ya Mei 29.

Waziri Mkuu Johnson aliambia SunSport: “Ligi ya Mabingwa Ulaya ni michuano mikubwa kabisa ya ngazi ya klabu kwenye soka la Ulaya. Na timu mbili za England zitacheza fainali, hivyo itakuwa aibu kubwa kama mashabiki watashindwa kwenda kuhudhuria.

“Itakuwa jambo zuri sana kama fainali itafanyika hapa. Nataka kuwasaidia mashabiki wa timu hizo zote mbili kupata fursa ya kwenda uwanjani kutazama fainali.”

waziri mkuu

Kiongozi huyo wa serikali ya Uingereza alisema mechi hiyo ikipigwa England, kutakuwa na uhakika wa mashabiki wapatao 15,000 kuhudhuria.


TENGENEZA FAIDA KUPITIA MCHEZO WA TITAN DICE UKIWA NA MERIDIANBET KASINO

Unapokuwa kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, huna sababu ya kucheza kwa mashaka. Titan Dice, ni mchezo unaweza kukupatia mamilioni kwa mzunguko mmoja!

SOMA ZAIDI

4 Komentara

    Amesema jambo jema ila sasa vipi kuhusu covid 19 imeisha au

    Jibu

    Dah sio poa

    Jibu

    Coronavirus sio poa

    Jibu

    Duuh sio poa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.