Soka la Uingereza linatajwa kama soka gumu la lenye mafanikio zaidi barani Ulaya. Lakini ni kweli? Xavi Hernandez atoa neno.
Xavi hajawahi kucheza soka la Uingereza lakini, amekutana na baadhi ya timu za EPL kwenye mashindano ya Ulaya. Pamoja na hilo, bila shaka anawafahamu baadhi ya wachezaji na malijendi wa soka la nchini humo.
Kwa uelewa wake na namna anavyoona mambo kule Uingereza, kocha huyu wa Barcelona ametoa neno lake akiwalenga zaidi wanahabari na wachezaji.
Kwa mujibu wa Xavi;
Uingereza, kama ukifanya vizuri kwenye baadhi ya vitu na kushinda baadhi ya michezo mfululizo, utaanza kuongelewa kama lijendi. Vyombo vya habari vinakuza sana vitu pamoja na kuwakuza wachezaji pasipo kustahili.
Huu ni mtazamo wa Kocha wa Barcelona lakini pia, kumewahi kuwa na maneno haya haya kutoka kwa wachezaji,makocha na wadau wa ligi zingine wakisema kuwa, mpira wa Uingereza haupo kama unavyosemwa na vyombo vyao vya habari. Wachezaji (hasa wa kiingereza) wanakuzwa kuliko uwezo wao kiuhalisia. Wapo wanaodai, hii ni sababu ya wachezaji wengi wa kiingereza kushindwa kufanya vizuri kwenye vilabu vya nje ya EPL.
SHAOLIN FORTUNES 100 ONJA LADHA YA USHINDI
Maana ya ushindi mkubwa ipo hapa katika mchezo wa SHAOLIN FORTUNES 100 ndani ya kasino maridhawa za meridianbettz. Kwa dau dogo unashinda zaidi, unaweza kucheza mara nyingi uwezavyo huku ukifurahia ladha ya ushindi.