Xavi na Barcelona walifikia makubaliano ya kuinoa timu hiyo yenye maskani yake kwenye jiji la barcelona nchini Hispania, ambapo Xavi alicheza kwa mafanikio makubwa.
Barcelona haikuchukua muda mrefu kuweza kumpata mrithi wa Koeman baada ya kufungashiwa virago vyake juzi jumatano, baada ya kupokea kichapo cha goli 1-0 kutoka kwa Rayo Vallecano.
Barcelona wameshakubaliana kila kitu binafsi na Hernandez, sasa imebaki uapnde wa Al Sadd kuweza kukubaliana kuhusu gharama za kuweza kuvunja mkataba wake na klabu hiyo ya nchini Qatar, Xavi bado ataendelea kuingoza klabu yake ya Al Sadd mpaka tarehe 3 Novemba huku akiwa kibarua cha mechi mbili za kuingoza Al Sadd .
Xavi anaweza kuanza kazi rasmi tarehe 6 Novemba dhidi ya Celta Vigo kwenye dimba la Banka Balaidos kama mambo yote yatakamilika mapema.

Sergi Barjuan kocha wa muda anatarajia kuingoza Barcelona kwenye mchezo wa kesho kwenye ligi kuu ya Hispania La Liga dhidi ya Alaves na wiki ijayo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Dynamo Kyiv.
Mchongo wa mkwanja mrefu kutoka kasino bora za mtandaoni za Meridianbet. Mchezo wa Circus Fever unakuweka katika nafasi nzuri ya kuwa mshindi. Furahia kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa meridianbettz.

CHEZA HAPA

