Yanga na TFF Ngoma Bado Nzito

Cliford Ndimbo, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) amesema kuwa Yanga SC wamegoma kuongea na kuacha barua licha ya kuitwa na Katibu Mkuu Wilfred Kidao.

Yanga na TFF Ngoma Bado Nzito

Juni 10 2025 TFF walitoa taarifa kuhusu ufafanuzi wa fedha za malipo ya zawadi ya bingwa wa CRDB Federation Cup ambazo Yanga SC walibainisha kuwa hawajapewa na katika barua hiyo TFF walieleza kuwa Yanga SC waliomba kwa maandishi fedha zao za ubingwa zikatwe moja kwa moja kwa malipo ya wachezaji wa kigeni.

Katika taarifa hiyo TFF iliwaambia Yanga SC wafike saa 4 asubuhi wakiwa na nyaraka zote za fedha ili kufanya ukaguzi.

Ndimbo amesema: “Klabu ya Yanga wamefika wameleta barua na kuondoka na wamesema hawana chochote cha kuzungumza, Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao alimuita CEO wa Yanga wazungumze alikataa.

“Hizi ni taasisi kubwa na sio kila jambo tunapaswa kuandikiana barua kama tunatoa posa. Kama CEO wa Yanga SC hajui bingwa anapata nini kwanini wanasema wanadai kiasi hicho cha fedha wanachosema.”

Yanga na TFF Ngoma Bado Nzito

Kwa upande wa CEO wa Yanga SC, Andre Mtine ameweka wazi kuwa wao ambacho wanahitaji ni hela ya ubingwa na sio kitu kingine.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

“Sisi hatutaki chochote zaidi ya zawadi yetu ya ubingwa kama kuna jambo lolote watuwasilishie kwa njia ya maandishi ila kwasasa hatuhitaji jambo lolote zaidi ya zawadi yetu ya ubingwa.
“Wewe umeshawahi kuona wapi Duniani kote hela ya madeni ikakatwa kwenye hela ya zawadi za ubingwa? Kwanza mnajua thamani ya fedha ya bingwa? Na wapi wametangaza thamani ya fedha za ubingwa?.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.