Mabingwa wa UEFA Europa Conference League klabu ya AS Roma wametangaza kumsajiri kiungo wa zamani wa klabu Manchester United Nemanja Matic aliyemaliza mkataba na klabu hiyo.
Kiungo huyo wa kimataifa kutoka Serbia mwenye umri wa miaka 33, alitangaza kuachana na klabu ya Manchester United mwezi April, kuwa baada ya msimu kuisha ataachana na klabu hiyo japo hakusema atakwenda klabu gani.

Nemanja Matic ameungana na Jose Mourinho kwa mara ya tatu, kwani alishafanya kazi nae akiwa Chelsea na Manchester United, kabla ya kujumuika nae tena kwenye klabu ya AS Roma ya nchini Italia inayoshiriki ligi ya Serie A.
AS Roma walitoa waraka wa kumtangaza Matic kwenye mtandao wao wa klabu uliosema, “klabu inafuraha kubwa ya kuthibitisha kumsajiri Nemanja Matic, mwenye umri wa miaka 33, kwa mkataba wa mwaka mmoja ambao utaisha mwezi June 30 2023.”
Matic nae aliongozea, “nashukuru na niheshima kubwa kujiunga kwenye kklabu hii na nina shauku ya kuanza msimu mpya na wachezaji wenzangu. Roma ni timu kubwa, ikiwa na mashabiki bora na kocha, Jose Mourinho ambaye anafahamika na kila mmoja wetu, maamuzi ya kuja hapa sikufikilia mara mbili.
“Natumai kwamba tutafanya kazi pamoja ili kufanikisha vitu vikubwa.”
ALIYA’S WISHES
Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.

