Gary Neville gwiji wa zamani klabu ya Manchester United amesifu uwezo wa kocha wa sasa klabu ya Tottenham hotspurs.
Gwiji huyo ameonesha kuvutiwa na kiwango kinachooneshwa na klabu hiyo yenye maskani yake jijini London ambayo anaamini uwezo ubora huo umechangiwa na ubora wa mwalimu huyo raia wa Italia, Hii inawezekana na uzoefu wa mwalimu huyo ndani ya ligi kuu ya Uingereza ambapo ameshafundisha klabu ya Chelsea pia ya jijini London ambapo pia amewahi kubeba ubingwa na Chelsea mwaka 2017.
Neville anaamini pia Conte kaleta hamasa na hali yaupmbanaji ndani ya klabu hiyo na kuongeza Conte amepata hamasa hizi kutoka kwa makocha kama Rafa Benitez na Jose Mourinho.
Ikumbukwe miezi kadhaa nyuma Neville alipinga uamuzi wa klabu yake ya zamani ya kutaka kumuajiri kocha huyo wakati mwalimu wa United wakati huo Ole Gunnar Solskjaer anafanya vibaya na hata pale alipofukuzwa kazi.

