Mauro Icardi Anulia Galatasaray.

Mauro Icardi nyota wa klabu ya PSG anakaribia kutua kwa vigogo wa soka nchini Uturuki klabu ya Galatasaray.

Nyota huyo raia wa Argentina inaelezwa ana uwezekano mkubwa wa kuachana na mabingwa haom wa ligi kuu ya Ufaransa baada ya kukaa hapo kwa muda na kushindwa kujihakikishishia namba ya kudumu.

mauro icardiIcardi aliyejiunga na klabu hiyo ya Ufaransa akitokea nchini Italia katika klabu ya Inter Milan amekua na wakati mgumu klabuni hapo chini ya walimu tofauti tofauti wanaopita klabuni hapo ambao wengi wamekua wakimyima muda wa kucheza mshambuliaji huyo.

Kocha wa klabu ya Galatasaray Okan Buruk amedai wako wanapambana kukamilisha dili la mchezaji huyo haraka iwezekanavyo kutoka kwenye klabu ya PSG.

Ni wazi Mauro Icardi anaamua kuondoka klabuni hapo kwenda kutafuta changamoto timu nyingine kwasababu ya ufinyu wa nafasi klabuni hapo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.