KMC Yasepa Lindi Kibabe

KIKOSI cha KMC chenye jumla ya wachezaji 20, Viongozi na Benchi la ufundi kimeondoka leo kuelekea Ruangwa, Lindi kwa ajili ya mchezo wa Ligi dhidi ya Namungo.

Akizungumzia hali ya kikosi, Ofisa Habari wa KMC, Christina Mwagala alisema: “Tunakwenda kwenye mechi yenye ushindani, lakini tumejipanga vizuri, tunawafahamu vizuri Namungo, licha ya ushindani kuwa mkubwa lakini kama Timu tunakwenda kwa tahadhari Ili kuhakikisha kwamba tunapata ushindi.

Siku zote hakuna mchezo mwepesi, michezo yote inahitaji maandalizi ya kutosha, jambo ambalo kama timu tumelifanya hivyo tunamuomba mwenyezi Mungu atufikishe salama Ili tukapambane uwanjani kupata alama tatu muhimu.

“Kwa upande wa hali za wachezaji wote wameondoka wakiwa salama, wana hali nzuri, wanamorali zaidi ya kutafuta ushindi kwenye mchezo huo muhimu.

Mashabiki na watanzania wote ambao siku zote wanaisapoti timu ni jukumu la kila mmoja kuwaombea wachezaji afya njema ili kuhakikisha burudani ambayo wameonesha kwenye michezo minne iliyopita inaendelea dhidi ya Namungo”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.