Kocha wa Manchester United Eric Ten Haag amesema itachukua miezi kadhaa ili klabu hiyo iweze kurudi kwenye ubora na kuwasha moto tena kama ilivyokua miaka kadhaa iliyopita.
Mashabiki wa Manchester United walianza kupata matumaini baada ya klabu kupata ushindi katika michezo minne ya ligi kuu Uingereza kabla ya kupewa kipigo cha aibu wikiendi iliyoisha dhidi ya mahasimu zao klabu ya Manchester City kitu kilichokuja kuchafua hali ya hewa tena klabuni hapo.
Vijana hao wa Eric Ten Haag jana walipata ushindi katika michuano ya Uefa Europa League kwa jumla ya mabao matatu kwa bila dhidi ya klabu ya Ommo Nicosia kutoka Cyprus huku wakikabiuliwa na mchezo mgumu dhidi ya klabu ya Everon katika ligi kuu ya Uingereza siku ya jumapili.
Kocha huyo wa zamani wa Ajax ameeleza timu yake itachukua muda ila kufikia kiwango anachokitarajia “Tumeiona timu dhidi ya Liverpool,Arsenal lakini ianatupasa kufanya tulichofanya kwa msingi thabiti,hilo ndo tunapaswa kulifanyia kazi kwasa”.
“Pia haitachukua siku, Itachukua wiki au miezi ili kuweza kusimamisha timu” Alifunguka Eric akielezea namna ambavyo timu hiyo inahitaji muda ili kufanya vizuri kwani yeye anaona sio jambo la haraka kuirudisha timu kwenye mstari.

