Eric Ten Hag kocha wa Klabu ya Ajax Amsterdam Jana alipokea kichapo cha 2-1 dhidi ya PSV Eindhoven katika fainali ya Kombe la KNVB la Uholanzi.

–
Kufuatia ushindi huo dhidi ya vijana wa Eric Ten Hag, PSV inakuwa klabu ya 3 kushinda kombe hilo mara 10+.
Ajax Mara 20.
Feyenoord Mara 13
PSV Mara 10
PSV Eindhoven imetwaa kombe hilo kwa mara ya kwanza kwa kipindi cha miaka 12.
Ajax Amsterdam inayonolewa na Meneja anayetajwa kuwa mbioni kuwa kocha mkuu wa Manchester United, Eric Ten Hag, ilikuwa ya kwanza kuona lango kupitia kwa Ryan Gravenberch mnamo dakika ya 23.
PSV Eindhoven ilicharuka na kupata magoli mawili ndani ya dakika 2 baada ya Erick Gutierrez (48′) na winga Cody Gakpo (50′) ambaye anawindwa na klabu ya Arsenal.

Ilikuwa siku mbaya kwa Ajax baada ya VAR kubatilisha magoli yake mawili.
Kipigo hicho kinamnyima Eric Ten Hag fursa ya kuchukua makombe mawili (Ligi kuu Uholanzi na Kombe la KNVB) Nchini Uholanzi kwa mara ya tatu.
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.