Kikosi cha Pan African baada ya kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Transit Camp kimeanza maandalizi yake kuelekea kwenye mchezo ujao wa ligi ya Championship dhidi ya Pamba.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Oktoba 22, mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyamagana, Mwanza.
Akizungumzia maandalizi yao, Ofisa Habari wa Pan African, Leen Essau amesema maandalizi yameanza baraka kutokana na muda kuwa mchache.
“Tulicheza jana jumatatu dhidi ya Transit Camp hivyo wachezaji hawajapata mapumziko na leo wameanza mazoezi ya kujiandaa na mchezo ujao.
“Kila kitu kipo sawa lakini licha ya ratiba kuwa ngumu tutaenda kupambana kwa ajili ya kuhakikisha tunachukua pointi tatu ambazo ni muhimu kwa upande wetu.”

