Winga wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya Brazil Antony imeelezwa amerejea ndani ya klabu hiyo baada ya kukosekana kwenye timu hiyo kwa takribani mwezi mmoja.
Antony amerejea ndani ya timu hiyo kutokana na taarifa iliyotolewa na Manchester United wenyewe na winga huyo ataweza kuanza mazoezi na timu hiyo na anaweza akawa kwenye machaguo ya timu kuelekea michezo inayofuta.
Katika taarifa ambayo Manchester United imeeleza kua mchezaji huyo ambaye alituhumiwa kutokana vitendo vua unyanyasaji kwa aliyekua mwenza wake, Atarejea ndani ya timu hiyo wakati uchunguzi ukiwa unaendelea zaidi.
Kutokana na taarifa ya klabu ya Manchester United inaonesha kua mchezaji huyo hajafanikiwa kumaliza kesi yake kutokana na tuhuma ambazo ameshutumiwa nazo wala kukutwa hana hatia kwakua uchunguzi bado unaendelea.
Kwenye taarifa ambayo wameitoa Man United kwa umma leo juu ya urejeo wa winga Antony bado wameendelea kuweka wazi kua, Hawaungi mkono vitendo vya unyanyasaji vyovyote kwani wanatambua athari ambazo zinatokana na unyanyasaji.

