Nyota mwa Manchester United, Romelu Lukaku ameweka bayana kuwa ni ndoto kuwa kweli siku moja akicheza soka kwenye Ligi ya Italia -Serie A!
Staa huyu raia wa Ubelgiji aliamua kuachana na soka la nchini humo na kusepea Uingereza mwaka 2011 akiwa kijana kabisa. Alichezea timu za Chelsea na Everton pia alienda kwa mkopo kule West Bromwich Albion kabla ya kwenda Manchester United mwaka 2017.
Staa huyu mwenye miaka 25 sasa, anasema katika siku za usoni angetamani kucheza soka katika Ligi ya Italia. Anatamani mno kupata nafasi kwenda kujijaribu huko. Lakini kwa sasa nyota huyu anasema anafikiria hatma yake pale Old Traffod.
“Kucheza Serie A ni ndoto, itakuwa ndoto kweli kweli. Natumaini nitaweza kucheza mapema au baadaye japokuwa kwa sasa akili yangu yote ipo Manchester United.” -Romelu Lukaku
Msimu huu Lukaku ameweza kucheka na nyavuy mara 15 kwa michuano yote.


aisha
ametisha sana
Furahav
Ucjal utaenda tu.
Povel
Haende kila la kheri