Tiemoue Bakayoko Aitamani Ufaransa

Nyota wa zamai wa Monaco Tiemoue Bakayoko ambaye ametumia msimu wake wa 2018/19 kwa kuwachezea AC Milan kwa mkopo ameweka bayana mapenzi yake ya kwenda kukipiga ufaransa. Nyota huyu anatarajiwa kurejea Chelsea kiangazi hiki wakati Milan wakionekana hawana mpango wa kumnunua moja kwa moja staa huyu.

Staa huyu bado ana mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Chelsea, klabu ambayo ipo katika joto la kuzuiwa kufanya usajili. Tiemoue Bakayoko anasema anatarajia kurejea Chelsea, lakini kiuhalisia angetamani kuwepo Paris.

Tiemoue Bakayoko Aitamani Ufaransa
Tiemoue Bakayoko Akiwa AC Milan

Alipoulizwa kuhusu hatma yake, anasema kuwa asingependa kuficha jambo lolote. “Ni kweli siku moja natamani nicheze Paris. Siwezi kudanganya kuhusu hilo. Ni kitu kikubwa kwangu na wapendwa wangu. Sisi ni Waparisi wa kweli.”

Akizungumzia ndoto yake hiyo ya kuchezea PSG, anasema atarejea Chelsea kumalizia mda wake. Alifanikiwa kucheza mara kwa mara akiwa chini ya Gennaro Gattuso lakini anakiri kuwa mwanzoni alikuwa na wakati mgumu sana klabuni hapo. Staa huyu anasema hawakuwa na uhusiano mzuri na meneja Gattuso.

3 Komentara

    Aende tu

    Jibu

    Aende akatimize ndoto zake ni sawa kwa kila mtu kua namatamio na nafasi ikitokea unatakiwa uitumie ipasavyo

    Jibu

    Aende mzee wa uchebe

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.