Inaonekana kwamba klabu ya Barcelona ipo mbioni kukamilisha dili la kumchukua nyota anayekipiga ndani ya klabu ya Atletico ambaye kwa kiwango kikubwa amekuwa sokoni kuwavutia mabingwa hao wa jiji la Hispania ambao kwa heshima kubwa wanataka kufanya biashara.
Mkurugenzi mkuu wa klabu ya Atletico, bwana Miguel Ángel Gil Marín amesema kwamba kwa sasa klabu hiyo inaweza kufanya biashara ya kupendeza ili kuuziana mchezaji huyo mwenye kiwango cha pekee sana kwenye soka ambapo wanaweza kunufaika sana kupitia nyota huyo.
Kwa siku za usoni amekuwa akihusishwa na kujiunga na klabu kubwa nyingi zikiwemo Manchester City, Manchester United, PSG na Barcelona wenyewe ambao kwa nafasi nyingine waliona nyota huyo angefaa kuwa sehemu ya kikosi hicho lakini inaonekana kwamba tayari maamuzi yamefikiwa kwa mchezaji huyo kujiunga Camp Nou.
Hii ni baada ya kipindi chake kirefu cha kufikiri kama angeweza kujiunga na klabu ipi ambalo lilikuwa ni jambo la muda mrefu sana kwake ila imeonekana kwamba klabu ya Barcelona inaweza kumchukua msimu huu lakini pia nao wanaweza kufanya mauzo ya Coutinho ili kuweka nafasi sawa japo yeye mwenyewe hana uhakika wa wapi atatua msimu ujao.
Kwa sasa yupo katika majukumu ya kitaifa akiwa anakiwakilisha kikosi chake kwenye Euro ambayo yatafanyika 2020. Hiyo ni sehemu kubwa kwa Griezman kuendeleza soka.
Gharama ya kumsajili nyota huyo inaonekana kupungua kutoka €200m hadi €120m kutokana na umri pia, ujirani uliopo baina ya wawili hao. Hivyo, kama atatua ndani ya klabu hiyo ataingia kwa heshima kubwa sana na atachangia mafanikio ya klabu hiyo kwa nafasi kubwa sana.
Lakini swali linalobakia ni kwamba, je, Griezman ataangusha wino wa kuendelea kusalia ndani ya Atletico kama ilivyo kawaida kwake kusema anaipenda sana klabu hiyo au ataweza kujiunga na mahasimu wake wa upande wa pili ili aweze kuwapa heshima ya mataji misimu mingine? Hilo ndilo jibu linalosubiriwa na kila mmoja kwa sasa.


Furahav
Barca inajua kuchagua vipaji.
Zeiyana
Usajil umekaa poa sana huo
Mwajumah
Asante kwa taarifa#Meridianbettz
Dorophina
Barca imefanya usajili wa uhakika kijana yupo vizuri sana
aisha
Barcelona hawakoseagi na wala hawana kazi mbovu mimi binafsi nawakubali barc
felister
habari njema kwa mashabiki wa barca
Tatu
Hasira za Jana Barcelona wanataka kusajili viungo
Nasra
Wapunguze jazba Barcelona
Caroline
Barcelona wapo vizuri kwenye iyo sekta
Mwanahamisi
Barca amefanya usajili wa uhakika
Issa
Griez anaweza kurudi nyumbani baada ya kutoonyesha kiwango bora barcelona
Fatina mfingi
Habar njema kwetu cc mashabiki
Warda
Hata wakisajili wesha lamba 8zao
Adelta
Barcelona poleni Sana Ila kwa sasa inabidi msajili upya@meridianbettz
lombo
mambo ni moto na meridianbet
Sabrina
Hizi ni habari njema
Saupha mohamed
Habari njema
Gabriel
Kwa upande wa Barcelona wanatakiwa kubadilisha kikosi kizima
Ester jackson
Kwa Jana Barcelona wameweka historia ya majozi poleni sana mashabiki ila tunawapa pongezi kwa hatua mnayo pigs ya usajili
Shafii
Gud news.
Samiah
Gud