Klabu ya Barcelona inamtaka Guardiola kurejea klabuni hapo! Mkataba wa sasa wa Guardiola na klabu ya Manchester City unaisha mwezi Juni 2021.
Guardiola amekuwa akihusishwa na kurejea klabuni Barcelona, na sasa Joan Laporta ambaye anatarajia kuwania nafasi ya raisi wa klabu ameweka wazi nia yake ya kutaka kumrejesha Pep Guardiola kutoka ligi ya Uingereza!
Laporta alishawahi kuwa raisi wa Barcelona mwaka 2003 hadi mwaka 2010, kipindi ambacho Guardiola alipandishwa hadhi kutoka timu ya vijana mpaka kufundisha timu ya watu wazima, mwaka 2008.
Laporta ametangaza nia ya kuwania uraisi wa klabu hiyo, na katika kitu anachokifikiria kuwafanyIa barcelona ni kumrejesha meneja amabaye amepata mafanikio makubwa katika soka kwa sasa, Guardiola.
Josep Bartomeu, raisi wa sasa wa Barcelona anaachia kijiti msimu ujao wa joto, na mchakato wa kumpata mrithi wake unaendelea.
Kwa upande wa Guardiola, ambaye mkataba wake unaisha Juni 2021, hatma yake imeendelea kuingia ukungu baada ya Man Cityn kupewa adhabu kwa kuvunja sheria ya UEFA ya manunuzi (kesi ambayo wameikatia rufaa)
Baada ya kuteuliwa na Laporta pale Barcelona, Guardiola alipata mafanikio kadhaa, akifanikiwa kushinda mataji matatu ya ligi na mawili ya ligi ya Mabingwa 2009 na 2011.

Katika kutangaza nia yake ya uraisi, alizungumzia mambo kadhaa kuhusu Guardiola
“Nitafurahi sana kurejea kwa Pep Guardiola, lakini yupo City sasa na ni uamuzi ambao atatakiwa kuufanya. Amekuwa ni mfano wa kila mtu anayehusika na Barcelona nafikiri mashabiki wengi watafurahia sana kama akirejea kuifundisha klabu tena.”
Barcelona wakiwa Chini ya Guardiola
3 – La Liga (2008-09, 2009-10, 2010-11)
2 – Ligi ya Mabingwa (2008-09, 2010-11)
2 – Copa del Rey (2008-09, 2011-12)
2 – Kombe la Dunia la Vilabu (2009, 2011)
2 – UEFA Super Cup (2009, 2011)
3 – Spanish Super Cup (2009, 2010, 2011)


Gabriel
Duuuh! Habar mpya
Lombo
dah iko poa iyo
Tahiya
Hiyo ni habari njema sana
Salma
Ni habari nzuri
Zeiyana iddi
Asanten meridianbet kwa taarifa
David pere
Akireje utakuwa ni vizuri Sana
Theckla
Barcelona wanazidi kuongea nguvu kwenye klabu yao wafanye wamchukue tu
Asia Abdy
Itapendeza
Aziza mushi
Akirejea itapendeza sana
theonestina
Namkubar Sana uyo jamaa.arud tu
Ernest
Ni jambo zuri sema tu nawasisi juu ya kizazi kilichobaki Barca kama kitarudisha heshima yake.
Emmy cleopa
Iko poa sana
Adelta
Asante meridian kwa taarifa
Mariam
Safi
Furahav
Kocha bora.
Shafii
Itakua poa Sana akirejea Barcelona
Mariam
👌👌👌👌
Hamidu
Coach bora muda wote anayejua kutengeneza timu yake. Akirudi barca atasumbua
Rehema
Habari Safi sn
Tatu
Ni vizuri
Agness
Nihabari njema
Sylvester
Guadriola kocha bora na ataweza kurudisha heshima ya Barcelona kama zamani…chaguo zuri
Neema juma
Ni vizuriii pia #meridianbet.
mwakalosi
Akirejea hatakuwa na makali yale aliyokuwa nayo hapo awali sio chaguo zuri
Mwajuma
Akifanya hivyo itakuwa poa
Povel
Hasirud Tena kwn ni mmoja aliyeweka heshima kwa kucheza na kufundisha klabu hyo mm natumain kwamb akirud hataaribu sifa zake Asante meridian bet# meridian bet#
aisha
barcelona wako vizuri kwa kuongeza jembe
Ester jackson
Karibu sana Barcelona
Elika
Guadiola ni kocha mzuri
Rehema Dickson
Safi sana kocha mzuri uyo
Amani
Me sizani Kama nijambo jema kurudi baka kwa sababu amekaa pale muda mrefu pia ametoka na heshima so anaweza akarudi alafu asiifikishe timu inapotakiwa akawa amevunja heshima yake#meridianbettz
Frank patrick
Namtabilia kufanya vibaya akirejea tena
Samiah
Asanteee meridian kwa taarifa
geniaskaluzwe8
Iko poa Sana #meridianbet
SADICK
Pep is successful football Manager. Thanks #MeridianbetTZ
khadija
itakuwa safi sana kama atarejea tena
Jenifer
Hii ni habari njema kwa Guardiola
Kenani
Sidhn km itawezekana ngoja tuone
Samira
Chaguo zuri sana kwa barcelona
felister
ni jambo nzuri kwa mashabiki wa barcelona
Fatina
Ni jambo
Lydia Emmanuel Magoti
Nijambo zuri
Devotha
Duuh asiende abaki man city
farida ahmadi
Habari nzuri Sana na njema pia hata mashabiki wake na wachezaji wake watafurahia
Theonestina
Itakuwa poa sana