Tetesi za Soka Barani Ulaya.


Tetesi zinasema Baba yake Lionel Messi ameiambia Paris St-Germain kwamba mshambuliaji huyo wa Barcelona na Argentina, 33, anataka kujiunga na Manchester City.

Messi alimpigia simu kocha wa Manchester City Pep Guardiola Jumanne iliyopita, kabla ya kuiarifu Barcelona kwamba anataka kuondoka klabu hiyo na kumwambia kuwa ”Nataka kushinda tuzo mbili za Ballon d’Or, na naweza tu kufanikiwa kutimiza hilo nikiwa na wewe”.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu amekataa kukutana na Messi kujadiliana kima chake na anashikilia kifungu cha kuwezesha uhamisho wake cha pauni milioni 624.

Chelsea imeonesha nia ya kutaka kumsajili mlinda lando wa Italia Gianluigi Donnarumma, 21, ambaye anasemekana thamani yake ni pauni milioni 50 lakini ameingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake na AC Milan.

Hatahivyo, AC Milan inafanya mazungumzo ya kumsajili tena mlinda lango wa Bournemouth Asmir Begovic baada ya kuwa na mchezaji huyo wa Bosnia, 33, kwa mkopo kuziba pengo la Donnarumma kwa kipindi cha nusu ya pili ya msimu uliopita.

Wakati huohuo, Chelsea huenda pia ikaongeza pesa zake za matumizi za msimu hadi zaidi ya pauni milioni 250 baada ya kufikiria kutoa ofa ya pauni milioni 80m kwa kiungo wa kati wa West Ham na England, Declan Rice, 21.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Jurgen Klopp aondoa uwezekano wa Lionel Messi kuelekea Liverpool lakini kocha wa Reds akubali kwamba raia huyo wa Argentina atakuwa na umuhimu mkubwa kwenye Ligi ya Epl.

Inter Milan iko katika hatua ya mwisho ya majadiliano ya pauni milioni 1.34 kumsajili beki wa kushoto wa Roma kutoka Serbia Aleksandar Kolarov, 34.

Tetesi zinasema Freiburg na mlinzi wa Ujerumani Robin Koch, 22, amefikia makubaliano binafsi na Leeds United.

Tetesi zinasema Kiungo wa kati wa Liverpool na Uholanzi Georginio Wijnaldum, 29, anawindwa na Barcelona.

Beki wa kulia wa Jamhuri ya Ireland Matt Doherty, 28, atafanyiwa vipimo vya matibabu na Tottenham Jumamosi baada ya kukubali kulipa kima cha awali cha pauni milioni 12 kwa Wolves. (Football London)

Mshambuliaji wa Senegal Sadio Mane, 28, yuko huru kuondoka Liverpool na kujiunga tena na aliyekuwa kocha wa Southampton Ronald Koeman Barcelona.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Aston Villa iko tayari kumaliza ushindani na Sheffield United na Fulham kwa kufikia makubaliano ya pauni milioni 12 ya beki wa kulia wa Nottingham Forest Matty Cash, 23.

Real Betis inamnyatia mlinda lango wa Chile Claudio Bravo, 37, ambaye sasa yuko huru baada ya kumalizika kwa mkataba wake na Manchester City mwisho wa msimu.

Kiungo wa kati wa Uhispania wa Under-21 Brahim Diaz, 21, anakaribia kujiunga na AC Milan kutoka Real Madrid.

Mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 29 aliamua kuikacha Barcelona kabla ya kushawishiwa kubaki na Meneja mpya wa timu hiyo Ronald Koeman.

Mshambuliaji wa zamani wa Sweden Zlatan Ibrahimovic, 38, amekubali mkataba mpya wa mwaka mmoja kusalia AC Milan, mkataba unaoaminika kuwa na thamani ya £6m.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Mshambuliaji wa Ureno, Cristiano Ronaldo, 35, amezima tetesi kuhusu mustakbali wake kwa kusema kwamba anajiandaa kwa msimu wa tatu Juventus.

Kuwasili kwa beki wa kulia raia wa Ireland, 28 Matt Doherty katika timu ya Tottenham kutoka Wolves kunaweza kuwa tiketi ya mlinzi wa Ivory Coast, Serge Aurier, 27, kuondoka.

Tetesi zinasema Tottenham imekataa ofa ya kwanza kutoka AC Milan kwa ajili ya Serge Aurier, huku Bayer Leverkusen ikionyesha nia ya kutaka huduma ya mlinzi huyo.

Tetesi zinasema Manchester United imewasilisha ombi la kumnasa kiungo wa Brescia Sandro Tonali, 20, ambaye anatajwa kama mmoja wa makinda wanaokuja juu nchini Italia.


Beti Mbio za Mbwa Mubashara

Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.

Cheza Hapa

42 Komentara

    barcelona wamuachie tu messi aondoke akapate changa moto nyingine

    Jibu

    Naona messi sasa anataka kuwa Manchester city pamoja na kocha Pep Guardiola kurudisha ndoto zake Mimi kama shabiki nasubiri tu kuona anakuwa wapi

    Jibu

    Kama kweli ni vizuri Messi kwenda man City akarudi kwenye chama lake la zamani wakashilikiane vizuri na guardiola

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Asante kwa makala

    Jibu

    Messi amekaa sana apo barca ni Bora sasa aende kwenye vilabu vyengine apate changamoto

    Jibu

    Kuna uwezekano wa mess kuamia man city

    Jibu

    Messi badili upepo na ww!

    Jibu

    Asante meridianbet Kwa taarifa

    Jibu

    Nazidi kufurahishwa na Leeds United jinsi wanavyofanya usajili ili kujipanga kwenye ushindani zaidi

    Jibu

    Nice information

    Jibu

    Aende kokote kila heri

    Jibu

    Asante kwa makala

    Jibu

    Akuna kingine Apo Messi ndio msema kweli Messi ndio mwenye uwamuzi wakuongea chochote kile yeye sehemu atakapo kwenda

    Jibu

    Maamuz ni yake mwenyew.

    Jibu

    Asantee kwa makala

    Jibu

    Muacheni aamue yeye mwenyewe maana kila siku naona kama anazungumziwa

    Jibu

    Haya magazet let’s see sehem gan mess ataend

    Jibu

    Shukurani kwa makala

    Jibu

    Messi maamuzi yake binafsi kuondoka hama kubaki Barcelona

    Jibu

    Messi gumzo mjini!!

    Jibu

    Akitua man city itakua Poa sana

    Jibu

    Ni mda mrefu kaitumikia barca kama akiona ni sahihi kutoka sawa as long as yy atakua poa

    Jibu

    Habari nzuri.

    Jibu

    Kwa Messi naona mahali sahihi pakwenda Ni man United

    Jibu

    Nice

    Jibu

    saf

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Messi kwa hatua hanayo haliyo fikia inaonesha zaili kabic hanampango na barcelona tena na ndio inavyo kuaga wachezaji mastar wanachagua wenyew kuichezea timu wanazo zipenda

    Jibu

    Wacha tuone

    Jibu

    Usajili ww mess utasumbua

    Jibu

    Good

    Jibu

    Messi hawezi kuondoka Barcelona

    Jibu

    Mie nasubilia tu ligi ianze

    Jibu

    Haya sasa tunasubili kuona messi Anelka wapi#meridianbett

    Jibu

    messi bora tu aende city

    Jibu

    Mess kuikacha fcb atavunja rekodi ya dunia kwa usajili

    Jibu

    tinasubil lig hianze

    Jibu

    Dirisha likishafungwa tutajua nani kaenda wapi nani kabaki.

    Jibu

    Naona messi sasa anataka kuwa Manchester city pamoja na kocha Pep Guardiola kurudisha ndoto zake Mimi kama shabiki nasubiri tu kuona anakuwa wapi

    Jibu

    Makala imekaa poa sana 👍

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.