Karibu Van de Beek, Ila kuwa Mpole Kidogo

Swali la kwanza la kujiuliza kwa Van de Beek ni anaenda kucheza nafasi gani? Jibu la swali la kwanza linaweza kuwa mwanzo wa swali la pili. Anakwenda kuchukua nafasi ya nani? Unakapokosa jibu la swali la pili, ndipo linapoibuka swali la tatu, kwanini Man United wamemsajili?

Msimu uliopita ameifungia Ajax mabao 13, akizidiwa na Hakimi Ziyech pekee. Alikuwa na wastani wa touches 7.8 kwenye box la wapinzani, ni zaidi ya mchezaji yoyote wa Man United kwa msimu uliopita. Zaidi ya yote, ni Bruno peke yake alifanikiwa kufunga, kupiga mashuti na kutoa assist zaidi yake. Ukitazama namba kama hizi, unawaza kwanini asianze katika kikosi cha United?

Unapojaribu kujijibu, linakuja swali, nani ampishe ili apate nafasi? Pogba na Bruno walitengeneza ‘muunganiko’ imara sana mwisho msimu uliopita. Ole Gunner Solksjaer hawezi kuwa kichaa kuwatenganisha tena.

Muhanga mkubwa anaweza kuwa Nemanja Matic. Donny ana wastani wa kupora mipira mingi zaidi ya viungo wote wa United. Isitoshe amewahi kucheza kama kiungo mkabaji, huenda Solksjaer anafikiria kumchezesha kama kiungo mkabaji, ili kumrahisishia majukumu Paul Pogba ya kuchezesha timu.

Pengine Ole anawaza kumtumia Doony kama mbadala wa viungo wake watatu. Ole anajua huwezi kubeba ubingwa bila kuwa na benchi imara. Liverpool walitwaa taji wakiwa na Keita na Milner nje, Guardiola alilitwaa akiwa na Mahrez nje. Ole hajasahau mateso aliyoyapata bila Pogba msimu uliopita. Anajua maana ya kikosi kipana.

Hata kama atapata nafasi katika kikosi cha kwanza, Van de Beek bado ana kazi ya kufanya. Viungo wachezeshaji wa Ajax hawajawahi kuwa na maisha mepesi ndani ya epl. Nishikie bia yangu wakati namkumbuka Davy Klaasen, nisogezee glasi wakati naitafuta picha ya Siem De Jong, kaa tuyajenge wakati naukumbuka mwanzo wa Christian Eriksen.

Donny anakuja akiwa bora ila ana kazi ya kupata nafasi katika kikosi cha United. Unahitaji muujiza kumpoteza Pogba au Bruno. Unahitaji moyo wa chuma kuchaguliwa mbele ya Matic. Bado tusisahau alipoishia Fred. Bado tusisahau alipoanzia Mctominay. Donny kazi anayo!


SHINDA NA HI LO

Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.

Cheza sasa

38 Komentara

    endapo juhudi zake na jitihada zikwa nzuri anaweza akapewa nafasi ya kucheza

    Jibu

    Asante kwa makala#meridianbettz

    Jibu

    Hapo ndio utakuwa balaa sana man u mana namba anazo cheza zina wababe wanzuri anakazi ya zuada kuwafanya wachezaji aliowakuta wampigie saluti ili kupata nafasi zaidi ya kucheza uwanjani

    Jibu

    Hapo inatakiwa juhudi na jitihada tyu mbona nafasi hatapata!!

    Jibu

    Apambane ili kufikia malengo.

    Jibu

    Tumkaribishe Kwanza mengine baadae yatajulikana.karibu Sana Van de Beek

    Jibu

    Van de beek anaweza kuchezeshwa kwa number yoyote na akafanya vizuri

    Jibu

    Hapa ndo wachezaji wengi huanza kujuta kwanini nimekubali kuja huku zaidi unakuwa hupati muda mwingi wa kucheza na kuishia bench tuu kwa muda mrefu

    Jibu

    mpk wamesajili mimi nadhani nafasi yake ipo ndo mana akasajiliwa

    Jibu

    Apambane ili afikie malengo yake

    Jibu

    Ajipange na aonyeshe juhudi atapata nafasi ya kucheza@meridianbettz

    Jibu

    Kila lakheri van de breek

    Jibu

    Vizuri akaribie Man U Sasa Apo picha linaanza namba zote Zina wenyewe alafu wababe wa kulisaka kabumbu Sasa Kaz ipo akikaza but anaweza akapata namba

    Jibu

    Kwa uchambuzi huu ina maana timu zinasajiri wachezaji ktk nafasi ambazo hakuna upungufu mkubwa#meridianbettz

    Jibu

    Cha msingi yeye inapaswa ajitume kwa dhati anapokua amepewa nafasi ya kucheza.

    Jibu

    Kutoa kwake ndio kutamsaidia

    Jibu

    Kila la kheri van de breek

    Jibu

    Van lete utam wa kiholanz united msimu huu watakaa tu

    Jibu

    Asante kwataharifa

    Jibu

    Kila la kheri#meridianbettz

    Jibu

    Sasa wamemsajili wa nn wakati hata namba ya kumpa hawajui?

    Jibu

    All ze best to him

    Jibu

    Jamaa anajua ndomaana kasajiliwa

    Jibu

    Pogba akiwa free plus bruno tutaona kitu kipya next season

    Jibu

    Hapo ni kupambana mwanzo mwisho

    Jibu

    Uyu jamaa noma anajua sanaa

    Jibu

    De beek ni kiungo ataeleta upinzan safu ya kiungo unitd

    Jibu

    Naaminii hatowaangushaa huko aendako

    Jibu

    Asanteee kwa taarifa

    Jibu

    Ajitahidi tu

    Jibu

    Asante kwa makala

    Jibu

    Asnt kwa taarif

    Jibu

    Big Deal

    Jibu

    Usajir mzur

    Jibu

    Kila lakheri van de breek

    Jibu

    Atapata tu nafasi

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.