Joao Felix ameuanza msimu mpya vyema kabisa na kocha Diego Simeone anatumaini mshambuliaji huyo wa Atletico ataendelea na kiwango hicho awamu hii.
Baada ya kutua akitokea klabu ya Benfica kwa dau la €126m, Joao Felix amehusika kwenye magoli mawili na asisti moja katika michezo sita aliyocheza msimu 2019-20 lakini anakumbukumbu yakupata majeraha mara kwa mara kitu kilichopelekea kutokuwa katika kiwango kizuri.
Atletico tayari wameuanza msimu mpya kwa kuikung’uta 6-1 timuya Granada katika mchezo huo Joao Felix alifunga goli lake la kwanza msimu huu kwa mkwaju wa penati pia alitoa asisti kwa Angel Correa.

Ingawa mchezo uliyofuata Atletico ililazimishwa sare ya kutofungana na timu iliyopanda daraja Huesca katikati ya wiki Joao alijaribu kupiga mashuti sita kwenye lango la Huesca na kutengeneza nafasi mbili kwa mchezaji mwenzake.
Diego Simeone ambaye ni bosi wa Atletico anatarajia kuona mengi kama hayo kutoka kwa mreno huyo na Timu yake itakutana na Villarreal katika dimba la Wanda Metropolitano siku ya Jumamosi.
“Msimu uliyopita kwenye pre-season alikuwa na kiwango kizuri ni sawa na hiki anachokionesha sasa,” Simeone alisema na waandishi wa habari siku ya Ijumaa.
“Katika michezo minne mitano alikuwa imara mpaka pale alipopata majeraha, alikuwa na mwanzo mzuri msimu ule.
Atletico ilipoteza michezo minne pekee katika LaLiga msimu ulliyopita na kutoa sare 16 na kumaliza nafasi ya tatu wakiwa nyuma ya mabingwa Real Madrid kwa alama 17.
Beti kwa Kitochi Kushinda 300,000,000!
Unajua kuwa unaweza kushinda milioni mia tatu kwa buku tu? Ndiyo! Unaweza kushinda kwa kupiga *149*10# na kubashiri. Ingia mchezoni!


Sauda
Aongeze mwendo, asirudi nyuma
magdalena
kijana anaendelea kupamba moto kila kukicha
Angelina
Akaze buti
Mwanahamisi
Akaze mwendo
Ernest
Joao Felix ni mchezaji mzuri sana kama ataendela kuwa katika ubora huu basi tutarajie kusikia mengi juu yake miaka ijayo
Dorophina
Joao ni mchezaji mzuri sana amekuja vizuri na anaspeed akiendelea ivyo atafika mbali
Fatina mfigi
Kaza buti kijan akikisha ashuki ng’oo
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Sana Simeone kaza buti utafika tuu jembe
Adelta
Felix Ni mchezaji mzuri sana
Elika
Ferix ni mchezaji mzur binafsi mimi namuelewa sana
Mwajumah
Akaze buti tu
Tatu
Diego simeone ategemee kushuhudia mazuri kutoka kwa mchezaji joao felix ambae alisajili kwa dau nono
Zeiyana
Diego yupo sahii kama atletico watamtumia vizuri Felix hatabadirisha matokea kwenye clabu hiyo maana amekua na moto wajabu
Nasra
Felix anafanyaga mabadiliko mara nyingi
Caroline
Joao felix usituangushe tunakuaminiaa
felister
akaze buti
Venerose
Safi sana inapendeza kijana
Hopemwaikuka
Itapendeza sana
Hidaya
Akaze buti
Issa
Simeone ana kikosi kizur sana felix ni moja ya wachezaj tumain kwa simeon
aisha
Felix yuko vizuri sana
Povel
Felix joa ngoj tuone
Amiri Kayera
Amekua kweny kiwango kizur
Rehema
Safi
Latifa juma mohamed
Akaze kamba Zaidi.
Saupha mohamed
Akazee
Gabriel
Felix ni mchezaji mzuri sana kama ataendela kuwa katika ubora
Rose kapinga
Nyota njema hiyooo
Sabrina
Itakua poa sana akiendelea vizuri zaidi
David Pere
Joao Felix ni mchezaji mzuri sana kama ataendela kuwa katika ubora huu basi tutarajie kusikia mengi juu yake miaka ijayo
Samiah
Safi