Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp amesema meneja wa Everton Carlo Ancelotti anaweza kuwa mshindani mkuu wa Liverpool katika Premier League.
Everton inaongoza katika jedwali la ligi ikiwa imeshinda mara nne katika mechi nne chini ya usimamizi wa raia huyo wa Itali ambaye aliajiriwa Disemba iliopita.
Wanacheza dhidi ya mabingwa Liverpool nyumbani Merseyside siku ya Jumamosi.

”Kile ninachofikiria kuhusu Carlo Ancelloti hakikuwa siri . Sikuweza kumuheshimu zaidi . Ni mtu mzuri” , Klopp aliambia BBC.
”Niliposikia kwamba atakuwa meneja mpya wa Everton , nilijua ushindani mkali mwengine umewasili Uingereza”.
”Walifanya biashara nzuri ya kununua wachezaji wakati wa dirisha la uhamisho la msimu uliopita. Walipata wachezaji waliowahitaji kuimarisha kikosi ambacho tayari kilikua kizuri”.
”Pamoja sasa ni kuzoea kile ambacho Anataka wafanye – kuwafanya kuwa bora zaidi”.
Ancelloti alimrithi Marco Silva kama mkufunzi wa Everton, baada ya kushinda mataji ya ligi akiwa Itali, Ujerumani, Ufaransa na England akiifunza Chelsea 2009-10.
Pia ameshinda mataji matatu ya ligi ya klabu bingwa Ulaya .Everton ambayo ilimaliza katika nafasi ya 12 katika ligi ya Premia msimu uliopita hawajamaliza chini ya nafasi ya saba tangu 2013 -14.

Baada ya kuimarisha safu ya kati katika dirisha la uhamisho la msimu uliopita baada ya kuwasajili wachezaji kama James Rodriguez, Allan na Abdoulaye Doucoure, wana matokeo ya asilimia 100% kutoka katika mechi saba katika mashindano yote msimu huu.
Wamefunga magoli 24 , mshambuliaji mpya wa England Dominc Calvert Lewin akifunga magoli tisa ikiwemo hatrick 2.
wachezaji wa Everton wakimkabili mchezaji wa Liverpool katikati
Klopp alisema: Calvert Lewin , Nilitaraji kwamba atapiga hatua kubwa katika miaka michache ijayo na amefanya hivyo, alisema Klopp.
”Ana kila unachohitaji kutoka kwa mshambuliaji , kimo, uwezo, malengo, kasi, mzuri angani anapofunga kwa kutumia kichwa na kumaliza na miguu yote”.
”Na sasa timu ina wachezaji bora – wingi zote mbili zina wachezaji huku James na Richarlison. Katika safu ya kati , Allan na yoyote anayecheza pale iwe Sigurdson ama yeyote yule”.
”Kwa kweli ni timu nzuri sana na safu ya ulinzi inafanya kazi yake vizuri kwasababu katika timu nzuri ni rahisi kujilinda nyuma”.
”Hicho ndio unachoona unapoitazama Everton hivyobasi itakuwa mechi ya kufana”.
Naam, hapa ni mahali pako! Kuwa shujaa kwenye sloti hii ya Samurai Ken ujishindie mkwanja na kujipa burudani murua.



Caroline
Everton kikosi chao kipo vizuri.laxima Klopp aogopeee
Mwajumah
Klopp kazi anayo apo
Lydia Emmanuel Magoti
Klopp ujipange Everton wapo moto
magdalena
everton imejipanga vya kutosha sana apo klopp kazi kweli anayo
zeiyana
evarton wamesajiri wachezaji wengi ili kukamilisha timu yao lakini hawana kikosi cha kuwazuia liverpool klopp hatoe wasiwasi
Gabriel
Klopp ujipange Everton wapo moto
Dorophina
Everton wapo vizuri wamejipanga
Tatu
Klopp ana kibarua kigumu msimu huu
Sauda
Kazi ipo
lombo
hatar
Mariam mtandama
Hatari
Povel
EVERTON wanajambo lao 2020/2021
Sabrina
Nouma sana
Issa
Kloop anajiham tu msimu huu ana chake
Hopemwaikuka
Balaa
Neema
Noma sana
Elika
Klopp bora amelijua hilo
Fatuma kasomo
Sio poa
Janeflora malisa
Hatar
Angelina
Mbona anajihami mapema
jullie
noma sana
Fatina mfingi
Safii
Adelta
Klopp jipange mpira hautabiriki
Amiri Kayera
Wakikutana inakuaga matoo
aisha
Pole sana kloop kwa kuwaagopa everton
Venerose
Hatari sana
Saupha mohamed
Nom as sanaa
Ernest
Everton wamekuwa wapambanaji sana msimu huu, lazima cheche zitoke
Tahiya
Kwer wanakutoa jasho