Tetesi zinasema mpango wa Real Madrid wa kumsajili mshambuliaji wa Paris St-Germain Mfaransa Kylian Mbappe, 21, hautavurugika hata mkufunzi wa klabu hiyo Zinedine Zidane akiondoka.
Zidane anasisitiza atakuwa na wachezaji hao hadi kufo licha ya tetesi kuibuka kuhusu hatma ya Mfaransa huyo Real.
Tottenham Hotspur imempatia mshambuliaji wa Korea Kusini Son Heung-min kandarasi mpya ya miaka mitano ya thamani ya £200,000 kwa wiki pamoja na marupurupu mengine, ambayo ni karibu mara mbili ya marupurupu ya anayolipwa katika kandarasi ya sasa itakayomalizika mwaka 2023.

Tetesi zinasema Mkufunzi wa Spurs Jose Mourinho anamtarajia Son, 28, kutia saini mkataba huo mpya hivi karibuni.
Ajenti wa Mesut Ozil anadai kuwa mkufunzi wa Gunners Mikel Arteta hakuwa mkweli kuhusu sababu ya kumuondoa mchezaji huyo waUjerumani katika kikosi chake.
Beki wa kushoto na nyuma wa Chelsea na Italia Emerson Palmieri, 26, huenda akaondoka Stamford Bridge mwezi Januari, huku Inter Milan, Roma na Napoli wakionesha dalili ya kuweka dao la kumnunua.

Manchester City wanajiandaa kumsajili winga wa Partizan Filip Stevanovic kwa kima cha £6m mwezi Januari dirisha la uhamisho litakapofunguliwa. Kiungo huyo wa miaka 18- raia wa Serbia aliwahi kuhusishwa na Manchester United.
Paris St-Germain wanajiandaa kumpatia Neymar mkataba mpya endapo wataafikiana na mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Brazil, 28.

Kiungo wa kati wa Chelsea na Italia Jorginho, 28, amesema yuko “tayari kushauriana” na Arsenal na kukiri kuwa Gunners wameonesha mpango wa kutaka kumnunua msimu huu wa joto.
Shirikisho la Soka nchini Uingereza limetishia kuzuia klabu za Uingereza kuwasajili wachezaji wa kimataifa kutoka nje ya Muungano wa Ulaya hadi pale Ligi Kuu zitakapo kubaliana kubuni sheria zinazowalinda wachezaji wa nyumbani baada ya Brexit.
Ondoka na Mkwanja Kwenye Tsh. 160,000,000
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu.


Elika
Mbappe kaza buti kambi popote
Khadija
Asante kwa taarifa meridian
Adelta
Kila la kheri mbappe
zeiyana
hana jituma sana ton heaung kwa kumuongezea mkata kwake kutalaeta mafanikio makubwa sana clabuni hapo
Mwajumah
Kambi popote tu mbappe
Carolyn
Asante kwa taarifa
Hopemwaikuka
Vyovyote itakavyo kuwa ni sawa tu
Lydia Emmanuel Magoti
Mbappe yeye ndio muwamuzi wa mwisho na Yeye ndio ujua nini anakifanya
Tatu
Mbappe ni mchezaji nyota kila timu inakuitaji
Sauda
Maisha popote
Povel
Nice update
Fatuma kasomo
Gud news
Issa
Habar njema
Saupha mohamed
Kila la kheri
aisha
Duuh mbappe
Sabrina
Itakua poa sana
Janeflora malisa
Hbr njm
Neema
Kila la kheri
warda
Tetesi ziko poa sana
Latifa juma mohamed
Imekaa njema.
David Pere
Mbappe yeye ndio muwamuzi wa mwisho na Yeye ndio ujua nini anakifanya