Maisha ni hatua na hatua moja huchagiza hatua nyingine. Baada ya kubeba taji la 7 la Formula 1, mkurugenzi wa Mercedes -Toto Wolff anatarajia kuanza mazungumzo na Lewis Hamilton kuhusu mkataba mpya.
Mkataba wa Hamilton unamalizika mwishoni mwa mwaka huu na hapakuwa na mazungumzo kuhusu mkataba mpya, hii ni kwasababu Toto Wolff na uongozi mzima wa Mercedes ulihitaji kumpatia muda Hamilton kufanyia kazi ndoto zake za kulisaka taji la 7.
Baada ya kumaliza mashindano ya Turkish Grand Prix na kubeba taji la Formula 1, Wolff anatarajia kuanza mazungumzo rasmi na Hamilton kuhusu mkataba mpya ndani ya siku chache zijazo.

“Kutoka kwenye ushindi wa 7 na kuanza mazungumzo ya mkataba mpya, hakutaitendea haki furaha ya mafanikio haya.
“Tutajipatia muda kidogo na kisha tutaanza huo mchakato. Mahusiano yetu ni zaidi ya biashara, ni mahusiano ya kirafiki na yenye kuaminiana.
“Hii siku moja ya majadiliano ni kati ya siku ambazo hatuzifurahii kwa sababu ni siku ambayo tunakuwaga na malengo tofauti. Biashara nzuri ni ile ambayo wahusika wanamalizana wakiwa hawajaridhika sana.” Alisema Wolff
Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.



Sauda
Hamilton makini sana
magdalena
aya mazungumzo na imani yataisha salama na kila kitu kitakaa sawa
Ester jackson
Jitahidi kupata saini yake muwepamoja zaidi
Adelta
Kila la kheri woff Kama watafikiah muafaka
Carolyn
Asante kwa taarifa
Ernest
Hamilton hapa atapiga mkwanja mrefu
zeiyana
Subiri tuangalie mwenyewe mahamuzi yake
Tatu
Kila la kheri kwake
Povel
Kila. La kheri Wolf Kama watafikiah .makubaliano
Mwajumah
Kila la kheri Wolff
Sabrina
Itakua poa sana kwake wolff