United Hawakutakiwa Kumuuza Lukaku

Manchester United waliamua kumuuza Romelu Lukaku kwenda Inter Milan kwa £74m. Uamuzi ambao baadhi ya wadau walishangaa na kuhisi ilikuwa ni makosa.

Moja ya watu ambao hawakuwaelewa United kwa nini waliamua kumuuza Lukaku, ambaye sasa ameendelea kung’ara Serie A ni Troy Deeney.

Nyota huyu aliondoka United msimu wa Joto wa 2019 kuungana na Inter Milan kwa ada iliyotajwa kuwa €74m baada ya kutumikia misimu miwili pale Old Trafford.

Nyota huyu alipokuwa United aliangaziwa sana na wakosoaji, lakini bado alifanya kazi nzuri akiondoka na magoli 42 katika mechi zake 96 alizocheza.

Lukaku Inter

Nyota huyu, amekuwa na stori nyingine na kuwa bora tangia alipoondoka United, akiwa na magoli 41 katika mechi 57 za michuano yote kwa Inter Milan, magoli 34 akiwa ameyapata msimu uliopita.

Lukaku pia amefanya vizuri katika ngazi ya Mataifa akiwa na timu yake ya taifa ya Ubelgiji. Ameshinda magoli 24 katika mechi 23. Alitoa mchango mzuri wa asisti katika mechi ya Jumapili dhidi ya Uingereza waliyoibuka na ushindi.

Troy Deeney anasema kuwa Lukaku hakuwa na rekodi mbaya kiasi cha United kuona ulazima wa kutemana naye. Anaamini United wana changamoto ya jumla ya ushambuliaji.

Troy Deeney Juu ya Lukaku

“Yuko vizuri sana, na wakati wote niliona ulikuwa uamuzi mgeni sana United kuamua kuachana naye.”

“Tangia ameenda Italia unaweza kuona upande wa ufundi wake na upande wa kocha, amekuwa bora maradufu. Ana kitu cha kuthibitisha.”


 

BASHIRI UKIWA MAHALI POPOTE!

Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.

Meridianbet Beti Popote

INGIA MCHEZONI!

22 Komentara

    Manchester united kwa sasa sijui wanakwama wapi?

    Jibu

    tatizo la united viongozi wake wanafanya mambo kwa kukulupuka sana awafikirii mbele

    Jibu

    Man u hamna kitu hapo

    Jibu

    Lukaku fundi

    Jibu

    Wanajutia hasaivi walimuona lukaku ameshuka kiwango kwenye mechi kadhaa wakaamua kumuuza bida yakumpa nafasi sasa hasaivi wanajutia inter Milan wanafurahia kutesa kwa zamu

    Jibu

    Man u hawajatuliza akili

    Jibu

    Lukaku jembe

    Jibu

    Lukaku Yuko vizuli

    Jibu

    Kweli kabisa walifanya makosa

    Jibu

    Nikweli Man U Wana suasua tena Lukaku akutakiwa kuzwa kwasababu kila mtu anajina kwenye krabu ana mamuzi ndio kilicho tokea hicho kwaio wasiongee tena kumkumbuka lukaku

    Jibu

    Walikosea sanaa

    Jibu

    Mzimu wa Lukaku utawasaka Man U tuu

    Jibu

    Man u aliofia mri wake lukaku hawakuangalia uwezo wake sasa wanajutia mahamuzi yao

    Jibu

    Kweli kabsa man u awaeleweki

    Jibu

    Mtian

    Jibu

    Lukaku ndio alikua mtu ambae anaibeba sana timu

    Jibu

    Hichi kitu nilijua tu man u kama wangejutia kwani wamemuuza jembe lukaku

    Jibu

    Kivuli cha lukaku bado kina watafuna manchester united

    Jibu

    Usajil wa lukaku kwa man ulikua mzur ila wakurugenz hawakumuamin sana

    Jibu

    Ni kweli ila hawakufukiria kwa Makin walikurupuk man U kwa kweli!!

    Jibu

    Man u watamtafuta lukaku na watajutia maamuzi yao

    Jibu

    Tatizo la man u wanakurupukaga

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.