Madrid wanakuwa wenyeji wa Barcelona kwenye El Classico wikiendi hii, mechi ambayo ina uzito mkubwa wa kuamua jambo kwenye mbio za taji La Liga.
Mechi hii pia inadhaniwa kuwa inaweza kuwa El Clasico ya mwisho kati ya makapteni wa timu hizo mbili, Lionel Messi na Sergio Ramos, ambao wamekuwa wakishiriki mechi kati ya mahasimu hawa wakubwa kwa kipindi cha takribani miaka 16.
Messi na Ramos, wote wako mbioni kumaliza mikataba yao, wakiwa wamesalia na chini ya miezi mitatu klabuni hapo. Wote wamekuwa huru kufanya mazungumzo na vilabu vingine tangia mwezi Januari. Imani ya Zidane ni kuwa watasalia Hispania.

Sintofahamu imetawala hatma ya wachezaji hawa ikiwa watasalia klabuni hapo, lakini kwa mujibu wa Zidane, bila shaka angetamani kuwaona wachezaji hao wote wakiendelea kuwepo La Liga.
Zidane amesisitiza kuwa anatambua aina ya mchezaji ya Messi, hata ikiwa atakuwa hafungi magoli, wanajua Messi ni nani, na wangetamani kama angeendelea kusalia Barca ili isiwe El Clasico ya mwisho kwake na Ramos.
INAWEZEKANA KUWA MILIONEA BILA KUVUJA JASHO NA KASINO YA ODD ONE OUT.
Odd One Out kutoka Meridianbet ni moja ya kasino maridhawa yenye picha halisi, ambayo inakupa nafasi ya kushinda kadri uwezavyo na kuwa milionea mara baada ya mzunguko kukamilika.



Adelta
Sijui kama itawezekana Messi kurudi Barcelona
Hopemwaikuka
Itakua poa tu
warda
Na hata huyo Messi mwenyewe hana mpango wa kuondoka